Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAWAKILISHI WA TANZANIA KATIKA MASHINDANO YA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE WASHEREKEA KUMALIZIKA KWA MASHINDANO HAYO.

 

Washindi wa Mashindano ya Guinness Football Challenge 2013 wakiwa kjatika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Epraimu Mafuru naMeneja wa bia ya Guinnes Davis Kambi wakati wa tafrija hiyo.
Regina Gwae kutoka kampuni ya R & R Associate akizungumza jambo na mmoja wa washiriki wa mashindano ya Guinness Football Challenge
Ilikuwa ni furaha tu kwa kila mtu.
Meneja wa bia ya Guinness Davis Kambi (kushoto) na Mkurugenzi wa Masoko wa SBL, Ephraim Mafuru wakiwa katika picha na wadau wengine wa Guinness na wafanyakazi wa SBL.
Wadau wa Guinness wakibadilishana mawili matatu wakati wa tafrija hiyo.
Meneja wa bia ya Guinness Davis Kambi akilamba picha na mabalozi wa kinywaji hicho.
Baada ya kumalizika kwa mashindano ya Guinness Football Challenge yaliyokuwa yakiendeshwa na Kupitia kipindi maarufu cha Guinness Football Challenge TV Show, hatimaye wawakilishi wa Tanzania katika mashindano hayo jana wamefanyiwa sherehe fupi katika Ukumbi wa Savannah Lounge Jijini Dar es Salaam na waandaji na wadhamini wa shindano hilo Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kuwapongeza kwa hatua waliyofikia.

Yaliyokuwa yakifanyika Afrika Kusini hatimaye yalimalizika hivi karibuni huku timu ya Tanzania ikiishia katika hatua ya nusu fainali kwa nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Ghana, Cameroon, Kenya na Uganda zilizoshiriki mashindano hayo ukiwa ni msimu wa tatu.

Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na wanahabari iliwashuhudia vijana walioshiriki mashindano hayo wakiwa na nyuso za furaha na kulakiwa kwa shangwe na uongozi wa Kampuni ya Bia ya Serengeti.

Akizungumza katika hafla fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa Savannah Lounge Meneja Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti,Moses Kebba ameipongeza timu hiyo kwa kufikia hatua nzuri ya mashindano hayo ambayo yalishirikisha timu mbalimbali za nchi zingine za Afrika.

Alisema kwamba katika hatua hiyo ya nusu fainali waliofikia ni dhahiri vijana hao wamefanya kazi nzuri huku akivishukuru vyombo vya habari kwa kuwatangaza vyema wakati wa ushiriki wao kati mashindano hayo ya Guinnes Football Challenge.

Amesema kwamba katika mashindano hayo nchi kadhaa zilishiriki kama vile Ghana, Cameroun, Kenya & Uganda, ambapo amekiri kwamba katika mashindano hayo kumekuwapo na ushindani mkubwa licha ya Tanzania kutoibuka na ushindi ilifanikiwa kufikia katika hatua ya nusu fainali.

Kwa upende wake Meneja wa bia ya Guinnes Davis kambi amesema kwamba wataendelea kusaidia zaidi kuibua vipaji vya soka kupitia ushiriki huo ambao utaleta tija katika soka la Tanzania kwa kutangazika hatimaye kufanya vyema katika mashindano hayo ambayo yamekuwa na umaarufu mkubwa Afrika na sasa wataendelea kutafuta zaidi vipaji vitakavyoshiriki katika msimu ujao.

“Kila mmoja katika kampuni yetu ya SBL na watanzania wanayofuraha na nakuwapongeza Daniel Msekwa na Mwalimu Akida, kwa kufanya vizuri licha ya kushindwa kufika hatua ya fainali lakini kazi mlioifanya imeonekana na mmeweza kuiwakilisha vyem Tanzania katika mashindano ya Guinness Football Challenge”, Alisema Kambi

Katika fainali ya mashinado hayo yaliyoshirikisha pia timu za Uganda na Kenya timu ya Tanzania ya GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE iliwakilishwa na Daniel Msekwa, Mwalimu Akida, Mohamed Kobembe, Gullam Sosha, Hamza Rashid,Lukwesa Kanakamfumu, Abubakari Mohamed, Kherry Sadallah, Simon Chimbo na Emmanuel Temu.

Akizungumzia mashindano hayo Daniel Msekwa amesema: “Tumepata uzoefu mkubwa katika mashindano lakini kubwa ni kuhakikisha tunafanya mambo kulingana na mawasiliano ya kupata vipaji zaidi ambapo timu za Kenya na Uganda zilifanikiwa kufikia malengo mazuri lakini hayo yote ni changamoto kwetu.”

“Tunaishukuru Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa sababu walifanya kila jitihada kipindi tupo Afrika Kusini kwenye mashindano na kuona utofauti wa nchi zingine kama Ghana na Cameroon,
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top