ecf843f57eec4b9c8c4e7a468c6e2584-7ffafe3b840f4226b9877892be2a722a-0_t607
Waziri Mkuu wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amezindua kampeni yake siku ya Jumapili, huku akilalamika kuwa hakuna mageuzi yaliyofanyika kuhakikisha uchaguzi wa Julai 31 unakuwa huru na wa haki.
Wazimbabwe watapiga kura katika muda wa chini ya wiki tatu, kuhitimisha serikali ya umoja kati ya Mugabe na Tsvangirai, ambao walilazimishwa kugawana madaraka baada ya machafuko yaliyofuatia uchaguzi wa mwaka 2008.
Tsvangirai alipata kura nyingi katika duru ya kwanza, lakini alijiondoa katika duru ya pili kutokana na wafuasi wake kufanyiwa vurugu na vyombo vya dola.
Rais Mugabe ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 33, alizindua kampeni yake Ijumaa iliyopita na kuwaambia wafuasi wa chama chake kuhakikisha ushindi wa kishindo