Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MJUE MZEE ABDULLAH ALRUWEIHY ALIYETEMBEA KWA MKUU KUTOKA DAR HADI TANGA. NO 2.

 


Akaulizwa nahodha mali hii ya nani?.Akasema ni mali ya Muhammed bin Habiib.Akaambiwa mtu huyu tunamtafuta siku zote,anakaa Tabora sehemu moja inaitwa Ndono kwa Mwanakurwa.
   Akaulizwa hii ni mizigo gani?.Akajibu hii ni tende.Akawaambia fungueni masanduku muangalie.Kufunguliwa wakakuta madebe mengine yana baruti na mengine yana risasi chini.
   Akakamatwa Yule nahodha akaambiwa sisi hatukupi nafasi yoyote.Akasema sawa lakini mimi nimeajiriwa tu.Mtu akikodi nipelekee mzigo wangu huu pahala Fulani,utajuaje ndani mna nini.Akaulizwa sasa utatufanzia taratibu tuweze kumpata mtu huyo?.Nahodha akajibu mtu huyu nimemuwacha Unguja.
  Akaambiwa tutakupa waranti  wa kumkamata.Akapewa waranti kwenda kumkamata Unguja.Alipofika sehemu moja inaitwa Kichwele pana wadokozi wakaivuta kwenye mfuko wakidhani ni pesa.Nahodha hakushtuka kuwa kilichovutwa ni waranti mpaka alipofika Unguja.
  Akaja mpaka Unguja.Alipofika Darajani yeye anaingia na marehemu baba anatoka Darajani.Wakasalimiana.Assalaam alaykum akajibu alaykum salaam.Aah nahodha!.Akamwambia hapa ulipo siwezi kukuwachia hata dakika moja.Umehatarisha maisha yangu.Umenambia ni mzigo wa tende kumbe baruti na risasi.Mimi nimekamatwa.Waranti huu hapa!.Akatia mkono mfuk
oni.Kutazama wapi! Waranti hana.
  Ikawa watu wote pale  wakawazingira.Kumwachia hataki.Watu wakamwambia ikiwa waranti huna rudi Darisalaama ukauchukue basi.Huyu muwache  hapa hapa.Ukija na waranti tutakupa mtu wako.Yule nahodha akasema InshaAllah.
   Baba akawaambia wale watu "Nyinyi mukumbuke kuwa serikali ya kiiengereza itaninyonga mimi.Akawaambia nipeni nafasi,wakamwachia.Akaenda mpaka sehemu moja panaitwa Chukwani akapata ngarawa ikamchukua mpka sehemu moja Dari salama panaitwa Tungi maeneo ya Kigamboni.
 Alipofika kule usiku.Pana mwarabu mmoja aitwa Saleh bin Suleiman katika nduguze.Jee namna gani kaka?.Akamwambia tafadhali kaka tafuta pa kwenda haraka.Hapa imekuja simu kuwa umeonekana Unguja ndipo hawa jamaa wakaondoka.
Sasa nifanze elimu gani.Akamwambia hapana elimu wala njia.Tukikwambia urudi Mascat haiwezekani.Hatuna njia ya kukupeleka.Baba akasema mimi nitakwenda Tabora.Utakwenda na nini?.Akasema Mungu atanipeleka.
  Akatoka akaja mpaka Morogoro,ana duka lake kaliweka.Akamkuta Hakim akamuuliz vipi?.Hakim akamwambia imekuja habari kuwa umeonekana Unguja na umekwishakamatwa ndipo askari wakaondoka lakini hawakutubakisha na chochote.
Swali:Walichukua vitu dukani?.
Jibu:Walichukua vitu vyote.
Akamuuliza sasa tutafanzaje?.Akamwambia hakuna njia.Mimi nakwenda Tabora.Akamwambia lakini na Tabora ni mbali Muhammed.Akasema Mungu atanisaidia.Basi kutoka Darisalaam  mpaka kufika Tabora alikwenda kwa siku 21.
Swali:Kwa miguu?.
Jibu:Allaahu a'alam matumizi aliyotumia lakini inajulikana ni siku 21 kwa miguu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top