Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MKUU WA WILAYA YA KILOLO GERALD GUNINITA ALIKOROGA , APANGIWA MAANDAMANO MAKUBWA ENDAPO RAIS KIKWETE ATAMNG'ANG'ANIA

 

mkuu wa wilaya ya kilolo Gerald Guninita

.....................................................................................................
 Wakati  wowote  kuanzia  kesho  chama cha wafanyakazi mkoa  wa Iringa  kinategemea  kutoa tamko dhidi ya mkuu wa wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Bw  Gerald Guninita anayedaiwa  kumkamata na kumweka mahabusu afisa usafiri  wa  wilaya ya Kilolo .


Taarifa ambazo mtandao  huu wa  ambazo umezipata  zinadai kuwa viongozi wa chama cha wafanyakazi kesho mapema asubuhi  kukutana  na wanahabari na kutoa tamko kali dhidi ya mkuu huyo wa wilaya ya Kilolo.

Mtandao huu umepata  kumtafuta mkuu  huyo wa wilaya kwa njia ya simu japo amedai kuwa si kila kitu ni habari  hivyo mtandao unasubiri kupata habari  toka kwa  viongozi hao  wa  wafanyakazi ili kujua undani wa sakata  hili ambalo kisa cha viongozi hao kutoa tamko ni baada ya mkuu wa wilaya kudaiwa kumkamata na kumweka mahabusu afisa wa usafirishaji wilaya ya Kilolo kwa kile alichodai kuwa ameshindwa kutoa usafiri wa kuwapeleka askari wa kumlinda nyumbani kwake .


Credits: www.francisgodwin.blogspot.com
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top