Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UZALENDO MASHAKANI!!! CHADEMA HAIPENDI AMANI YA NCHI ..... YASUSIA MJADALA WAKE

Na Abdallah Khamis

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekataa kuhudhuria mkutano wa siku mbili wa kujadili amani ya nchi, ulioitishwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kwa madai kuwa hauna tija kwa taifa.

Chama hicho kimetaka fedha zitakazotumika katika mkutano huo unaofanyika katika Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam zielekezwe katika shughuli za kimaendeleo, ambazo zitakuwa na tija kwa wananchi wengi.

 
Msimamo huo ulitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo, Benson Kigaila, wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo alisema wamesusia mkutano huo kwa sababu waandaaji wamewaalika wanasiasa pekee, wakati suala la amani halishikiliwi na wanasiasa pekee.

Kigaila alisema CHADEMA inaamini jukumu la kulinda amani linashikiliwa na makundi mbalimbali ya kijamii, hivyo wanapaswa kushirikishwa katika mkutano huo.

 
“Kikubwa ni kwamba Mwenyekiti wa TCD, James Mbatia, amekiuka maazimio ya kikao ya kuteua muwezeshaji wa mkutano huo na badala yake akafungamana na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuteua watu wanaowataka. Pili, amani haijadiliwi… amani inatengenezwa na kuwapo mazingira ya haki na usawa,” alisema Kigaila.

 
Alisema licha ya serikali inayoongozwa na CCM kulalamikiwa kuwa nyuma ya mikakati ya kuvuruga amani na kutolea mfano kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ya hivi karibuni kuwa wanaokaidi amri za vyombo vya dola wapigwe bila kujali kuwa wanatetea haki zao za msingi.


 
“Tunafahamu amani si ya wanasiasa peke yake, ni ya wadau mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini, taasisi za kiraia na zile zisizo za kiserikali, hao hawakushirikishwa, sasa tunakwenda kujadili suala hili na nani au wale wanaoamrisha wananchi wapigwe?” aliongeza.

 
Alisema kuwa mchakato huo hauendani na hali halisi iliyopo sasa, ambapo serikali ndiyo inayolalamikiwa kutesa na kuwadhuru baadhi ya watu huku ikishindwa kuunda tume huru ya kimahakama kufuatilia mchakato huo.

Kigaila alisema kama CHADEMA ingekubali kuhudhuria ni sawa na kufanya sherehe juu ya makaburi ya watu waliokufa katika mikono ya serikali ya CCM, jambo ambalo CHADEMA haiwezi kulikubali.

 
Alisema kwa sasa kuna matukio ya kutatanisha yakiwahusisha maofisa wa polisi, ikiwamo kuuawa kwa aliyekuwa mtangazaji wa kituo cha televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi, mlipuko wa bomu Arusha, kutekwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, Absalom Kibanda na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Stephen Ulimboka.


Kigaila alisema matukio hayo yote licha ya kuvihusisha vyombo vya dola mpaka sasa serikali imekaa kimya na inaendelea kujificha katika mgongo wa vyama vya siasa.

 
Alibainisha kuwa wakati leo mkutano huo ukianza jijini Da esSalaam, mkoani Mtwara kuna malalamiko ya wananchi kupigwa, kubakwa na kuteswa na baadhi ya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) bila kuchukuliwa hatua za kisheria.

“Matukio yote haya yanatuonyesha serikali haina dhamira ya kutaka amani iendelee, imeamua kubagua watu wa kuhudhuria mkutano huo…sisi hatukubaliani nayo,” alisema.

 
Kigaila alisema wana taarifa kuwa serikali imefadhili mkutano huo utakaotumia sh milioni 400 kwa siku mbili na idadi ya wajumbe watakaohudhuria ni watu 70.

TCD waijibu

 
Tanzania Daima, liliwasiliana na Mwenyekiti wa TCD, James Mbatia, juu ya mkutano huo kufadhiliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambapo alikanusha mkutano huo kuandaliwa na serikali kwa mgongo wa TCD.

 
Mbatia alisema mkutano huo unafanyika kutokana na maazimio ya vyama vyote vilivyokutana mjini Dodoma Februari 7, mwaka huu na kukubaliana wafanye mkutano wa kuzungumzia masuala ya amani inayoonekana kulegalega kwenye baadhi ya maeneo.

 
Aliongeza kuwa si kweli kuwa wameyatenga makundi mengine, bali vikao hivyo vitakuwa vya mwendelezo wa makundi mbalimbali na hivi sasa wameanza na wanasiasa.

 
Alisema mkutano huo unaoanza leo kutakuwa na mada nne tofauti, ambazo ni amani na demokrasia, amani na usalama itakayowasilishwa na IGP Mwema, nafasi ya vyombo vya habari katika kuenzi amani itakayowasilishwa na Dk. Ayoub Ryoba, pamoja na uzoefu wa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.


Chanzo - Tanzaia Daima
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top