Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

AHUKUMIWA KUNYONGWA MPAKA KUFA BAADA YA KUMUUA MAMA YAKE MZAZI KWA MAKUSUDI HUKO TABORA..!!

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Tabora imemhukumu mtu mmoja kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mama yake mzazi kwa makusudi.
Akitoa hukumu hiyo katika kikao chake kinachoendelea Nzega iliyochukua zaidi ya dakika 45, Jaji Amiri Mruma alisema mahakama imeridhika na ushahidi uliowasilishwa dhidi ya mtuhumiwa James Okoko (51) mkazi wa Nzega mjini.
Jaji huyo alisema kutokana na kukithiri kwa vitendo vya mauaji ya kikatili pamoja na kushambulia kwa mapanga bila sababu na kujichukulia sheria mkononi ametoa hukumu hiyo ili iwe fundisho kwa watu wenye nia kama hizo.
Awali wanasheria wa serikali Ildephonce Mkandara, Grace Muwange na Monica Mlao waliiambia mahakama hiyo kuwa mtuhumiwa alimpiga mama yake mzazi Catherine Mihambo hadi kufa kwa kutumia fimbo na stuli aliyompiga nayo kichwani baada ya kukatazwa kula chakula cha mchana kutokana na utovu wa nidhamu, tukio hilo lilitokea Septemba 23 mwaka 2008.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top