Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Usafiri kituo cha Ubungo sasa ‘poa’

Abiria waendao mikoa mbalimbali wakiwa katika stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani ya Ubungo. 
*******
Hali ya usafiri katika Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Ubungo,  imerejea kuwa ya kawaida.
 Kwa takribani wiki moja ,kituo hicho kilikuwa katika hali mbaya ya usafiri, kutokana na kupungua kwa mabasi ya kwenda mikoani.
Mwananchi jana ilikwenda kituoni hapo na kushuhudia idadi ndogo ya  abiria huku mabasi yakiwa mengi.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Ofisa kutoka Chama cha Kutetea Abiria Tanzania (Chakua), Gervas Rutabuzinda, alisema hali ya usafiri imerejea kama zamani.
“Tunashukuru Mungu hali ya usafiri imerejea kuwa ya kawaida,” alisema Rutabuzinda
Rutabuzinda alisema baada ya kumalizika kwa sikuku za mwisho wa mwaka tatizo  tatizo la usafiri litahamia mikoani, kwani abiria wengi watakuwa wanarejea Dar es Salaam.
 
MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top