Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

CUF NAO PIA WAZINDUA KAMPENI ZA JIMBO LA KIEMBE SAMAKI.

 

01Baadhi ya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Chama hicho Professa Ibrahim Haruna Lipumba katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki  katika kiwanja cha Bustani ya Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi Unguja.02Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Professa Ibrahim Haruna Lipumba na viongozi wengine wa chama hicho wakirusha maputo kama ishara ya uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki uliofanyika Bustani ya Kiembesamaki, Wilaya ya Magharibi Unguja.
03Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Professa Ibrahim Haruna Lipumba akimnadi mgombea wa Chama hicho katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki, Abdulmalik Haji Jecha, katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki zilizofanyika Bustani ya Kiembesamaki, Wilaya ya Magharibi Unguja.Picha na Makame Mshenga Maelezo Zanzibar.
Na Miza Kona – Maelezo
Mwenyekiti wa chama cha Wananchi CUF Taifa Profesa Ibrahim Haruna Lipumba amewataka wananchi wa Jimbo la Kiembesamaki kumchagua kiongozi atakayeweza kuingia katika bunge la katiba na kuyatetea na kuleta maslahi ya Zanzibar.
Kauli hiyo ameitoa jana huko Kiembesamaki wakati alipokuwa akizindua kampeni na kumtambulisha mgombea uwakilishi kupitia chama hicho.
Amesema kiongozi bora ni yule atakaeweza kuitetea Zanzibar na kuipatia maendeleo na kupata mamlaka yake kamili pamoja na  kuleta mabadiliko.
Aidha ameeleza kuwa CUF inataka kuleta mabadiliko katika mambo ya muungano na kuona kuwa haki inafanyika katika nchi zote.  
Aidha amesema kupita chama cha CUF wananchi watapata kiongozi mzuri atakaeweza kuingia kwenye bunge la katiba na kuitetea nchi bila ya woga wala kupoteza mwelekeo.
“Mpeleke mtu atakaeweza kuingia kwenye bunge la katiba na kutetea maslahi ya Zanzibar”, alifahamisha.
Hata hivyo amesisitiza kuwa uchaguzi ufuate utaratibu uwe huru na haki bila ya kushirikisha vyombo vyengine.
Nae mgombea uwakilishi AbdulMalik Haji Jecha amesema pindipo wananchi watamchagua ataitetea Zanzibar kwa moyo wa uzalendo na kuleta maendeleo kwa maslahi ya nchi.
Uchaguzi huo mdogo wa jimbo la Kiembesamaki unafanyika kutokana na aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo hilo Mansour Yussuf Himid kuvuliwa uwanachama kupitia CCM
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top