Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

FAHAMU UKWELI ULIVYO JUU YA ASKARI POLISI ALIYEJIPIGA RISASI MKOANI SHINYANGA...!!



PC David Alfred
Akizungumza na waandishi wa habari leo Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Evarist Mangala amesema tukio la askari wake aitwaye David Alfred (25-30)kujeruhiwa kwa risasi limetokea jana majira ya sa 12 na nusu jioni wakati askari huyo akikagua silaha aina ya SMG katika ghala la silaha katika  kambi ya jeshi la polisi mjini Shinyanga ili aingie kazini.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga akizungumza na waandishi wa habari mapema leo kuhusu tukio la askari kujeruhiwa kwa risasi
Amesema wakati askari huyo akikagua silaha hiyo ghafla risasi ilifyatuka na kumjeruhi chini ya bega la mkono wa kushoto hali iliyopelekea akimbizwe katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya matibabu. 
Amesema tukio hilo ni bahati mbaya tu huku akiwataka askari polisi kuwa makini na kujali usalama wao kwanza kabla na wakiwa kazini.
Dkt Fredrick Mlekwa akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake

Mganga mfawidhi wa Hospitali ya mkoa Shinyanga Dkt Fredrick Mlekwa amesema hali ya majeruhi huyo inaendelea vizuri anaongea, vizuri  na kwamba kufuatia tukio hilo askari huyo amepata majeraha katika sehemu za kifuani na mkono wa Kushoto.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top