Na Demetrius Njimbwi na Alexander Mpeka, Jeshi la Polisi
……………………………………………………………………………
Jeshi la Polisi Nchini limesema
kuwa, litamchukulia hatua kali mtu ama kikundi chochote katika jamii
chenye lengo la kutaka kuvunja, kuhatarisha amani au kuwa sehemu ya
uhalifu jambo ambalo ni kinyume cha sheria za nchi.
Kauli
hiyo imetolewa jana na kamishna wa Polisi Jamii Nchini (CP) Mussa Alli
Mussa, wakati wa mkutano wa maofisa wa Polisi pamoja na askari wa vyeo
mbalimbali uliofanyika katika mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, jijini Dar
es salaam.
Kamishna
Mussa, alisema kuwa, kutokana na kupungua kwa matukio ya uhalifu na
wahalifu, kumechangiwa zaidi na uelewa wa wananchi pamoja na kushiriki
kwao katika dhana nzima ya Polisi Jamii/Ulinzi Shirikishi jambo ambalo
kwa sasa limeifanya jamii kuishi kwa amani.
Hata
hivyo, kamishna Mussa, aliwataka askari kuongeza ufanisi katika
kuwahudumia wananchi ikiwa pamoja na kuwataka wananchi na wadau
mbalimbali wa Polisi Jamii/Ulinzi Shirikishi kuendelea kushirikiana na
Jeshi la Polisi pamoja na kufichua mitandao ya uhalifu.
Kwa
upande wake Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Lazaro Mambosasa,
amewataka askari pamoja na watendaji wa Jeshi la Polisi kutokujitenga
katika kueneza dhana ya Polisi jamii/Ulinzi shirikishi na badala yake
wajikite zaidi katika kutoa huduma bora kwa wananchi ili kuisaidia jamii
kuondokana na changamoto za matukio ya uhalifu na wahalifu.
Post a Comment