Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MOTO WATEKETEZA FAMILIA NZIMA

 
Siku moja baada ya watu 25 kuripotiwa kufa kwa ajali tofauti nchini ikiwamo iliyoua familia mkoani Singida, familia nyingine ya watu wanne imeteketea kwa moto ndani ya nyumba katika Kijiji cha Iputi wilayani Ulanga mkoani Morogoro.
Pamoja na tukio hilo, imeripotiwa kuwa watu wengine 10 wamefariki dunia katika matukio tofauti ya ajali zilizotokea katika mikoa ya Arusha, Dodoma na Singida.
Matukio hayo ni mwendelezo kwa mwaka 2014 kuanza vibaya baada ya vyombo vya habari jana kuripoti vifo vya watu 15 katika ajali tofauti zilizotokea Same mkoani Kilimanjaro, Singida na Lindi.
Moto waua wa Morogoro

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alisema kuwa familia ya watu wanne ya baba na watoto watatu, iliteketea kwa moto uliotokea saa 7 usiku juzi katika Kijiji cha Iputi wilayani Ulanga.
Shilogile aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Kasmu Maleo (42), Kumbukeni Maleo (5), Mwanaisha Maleo (4) na Alfa Maleo (2).
Alisema kuwa katika ajali hiyo mama wa watoto hao, Kisia Kihina (35), alijeruhiwa vibaya na moto na amelazwa katika Kituo cha Afya cha Mwaya akipatiwa matibabu.
Kamanda Shilogile alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni moto ulioachwa na familia hiyo baada ya kupika chakula cha jioni, hivyo ukateketeza nyumba hiyo.
Wafukiwa na kifusi Karatu
Katika tukio jingine, watu sita walifariki dunia baada ya kufunikwa na kifusi wakati walipokuwa wakichimba changarawe wilayani Karatu mkoani Arusha.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Japhet Lusingu alisema kuwa tukio hilo lilitokea saa 10:00 juzi jioni katika Kitongoji cha Sumawe Wilaya ya Karatu mkoani Arusha.
Aliwataja waliokufa kuwa ni John Oswald (22), Tumaini George (23), Benjamini George (16), Rafael Robet (23), John Jumanne (28) na Emmanuel Oswald (33) wote wakazi wa Sumawe wilayani Karatu.
 
MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top