Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Msuya aeleza wezi walivyomwibia

Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya (pichani) ameeleza alivyoibiwa mtandao wa miundombinu ya umwagiliaji na bomba za maji 80 katika shamba lake lililopo katika Kijiji cha Chomvu Usangi, wilayani Mwanga, Kilimanjaro.
             
Hatua hiyo imekuja baada gazeti hili kuandika habari za Polisi wilayani Mwanga kufanya operesheni ili kuwasaka watuhumiwa wa wizi huo wa mabomba hayo yenye thamani ya Sh2.4 milioni.

Hata hivyo baadhi ya wakazi wa wilaya hiyo walilalamikia operesheni hiyo kwamba baadhi ya watu wamekuwa wakikamatwa wakati hawahusiki.

Taarifa iliyotolewa na Msuya jijini Dar es Salaam, jana ilisema, usiku wa Septemba 20, 2013, watu wasiojulikana waliingia shambani kwake na kuharibu mtandao wa umwagiliaji maji zikiwemo bomba 80.

Msuya alisema licha ya mtandao huo wa bomba kufukiwa ardhini kwa zege bado wahalifu hao walifanikiwa kuzing’oa na kuondoka nazo.

“Uharibifu na wizi huu ni mkubwa na mahali pengine walitumia misumemo ya chuma kukata mabomba na kuyaachanisha na zege,” alisema.


Alisema Septemba 21, 2013 taarifa za uhalifu huo zilifikishwa kwa watendaji wa Kijiji cha Chomvu, Kata ya Chomvu, Tarafa ya Usangi na hatimaye uongozi wa Polisi wa Wilaya ya Mwanga na Mkoa wa Kilimanjaro.

“Nilipokuwa nyumbani wilayani Mwanga, wakati wa Krismasi, nilipata maelezo kutoka kwa maofisa wa polisi kuhusu maendeleo ya upelelezi wa uhalifu huu,” alisema Msuya.

Aliwapongeza Polisi kwa kazi wanayoendeea kuifanya licha ya kuwa katika mazingira magumu na kusema kwamba ana imani wahalifu hao watakamatwa wakiwa na vidhibiti ili waweze kufikishwa mahamani.

Alisema Tanzania inaongozwa na kutawaliwa na sheria na kwamba viongozi wanashauriwa kuwatia moyo polisi kwa kazi ya kupambana na uhalifu nchini.

Msuya alisema wasipofanya hivyo uhalifu wa aina hiyo unaweza kusambaa na kutokea sehemu nyingine kitendo ambacho hakikubaliki.

Juzi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alikaririwa akithibitisha kutokea kwa tukio hilo nyumbani kwa Msuya na kutahadharisha watu wasipotoshe uchunguzi huo.

MWANANCHI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top