Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MUME AMNYONGA MKE NA KUTUTUMBUKIZA CHOO CHA KANISA

 

Watu watatu wafariki dunia mkoani Iringa katika matukio matatu tofauti likiwemo la John Kaguo (30) mkazi wa Usokami kumuua mkewe bi Jane Makombe (25) mkazi wa Lutuna kwa kumnyonga shingoni na kisha kumtumbukiza kwenye choo cha kanisa.
 
Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 25 januari usiku huko maeneo ya kijiji cha Ihalimba kata ya Ihalimba tarafa ya Kibengu wilaya ya Mufindi.
Mungi alisema mtuhumiwa huyo amekamatwa kwa mahojiano Zaidi huku chanzo cha tukio hilo la kinyama likichunguzwa.
 
Na katika tukio lingine bi Neema Luwumba (33) mkazi wa Lugalo alifariki dunia katika Hospitali ya mkoa alipokuwa akiendelea na matibabu baada ya kupigwa na shoti ya umeme maeneo ya Mkimbizi.
Kamanda Mungi alisema marehemu alikutwa na janga hilo la kupigwa na shoti alipokuwa akianika nguo alizokwisha kuzifua katika kamba inayosadikika kuwa ni waya wa umeme.
 
Mbali na matukio hayo mawili, Kamanda Mungi alisema mwanaume mmoja jina Juma Cheles (60) alifariki dunia baada ya kugongana uso kwa uso na pikipiki  huko maeneo ya kijiji cha Nzivu Mafinga wilaya ya Mufindi.
 
Marehemu alikuwa akiendesha pikipiki aina ya sunlg yenye namba za usajili T 609 BHJ aligongana na pikipiki yenye namba za usajili T 268 BZR Sunlg mali ya Benedict Mwanjombe (30) na kufariki papo hapo, huku chanzo cha ajali hiyo kikiwa ni mwendo kasi.
Mwandishi wa mtandao   www.matukiodaima.com Diana Bisangao kutoka Iringa anaripoti kuwa
 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top