Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Walichokisema Bakwata juu ya wanaopora kwenye misikiti.

    
ijumaa-mosque
Baraza kuu la waislamu Tanzania (BAKWATA) limekemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya waumini wa dini hiyo ya kuvamia na kupora misikitini na kusbabisha uvunjifu wa amani,akitoa salam za baraza hilo kwenye Baraza la Maulid lililofanyika mjini Kigoma, Naibu Katibu
Mkuu wa BAKWATA, Sheikh Mohamed Khamisi amesema kuwa vitendo vya uporoaji wa madaraka kwenye misikiti na umwagaji damu ni kinyume na muenendo na mafundisho ya dini.
Kutokana na hilo amesema kuwa   baraza hilo halina budi kukemea kwa nguvu vitendo hivyo na kuwaonya waislam kuacha mara moja kwani vimekuwa vikiipaka matone na kuunajisi uislam.
Akizungumzia jambo hilo kwa niaba ya serikali Mkuu wa mkoa Kigoma, Issa Machibya amesema kuwa serikali haitasita kuwachukulia hatua kali watu wote watakaobainika kuhusika katika vitendo vya uporaji madaraka na kufanya mapinduzi kwenye
misikiti na kupelekea uvunjifu wa amani na umwagaji damu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top