Kamishna
Jenerali wa Magereza Nchini Namibia(hivi sasa Mstaafu) wa kwanza kulia
mstari wa pili akikagua Gwaride Maalum lililoandaliwa na Maafisa
Magereza wa Nchini Namibia katika sherehe za kukabidhi Madaraka ya
Uongozi wa Jeshi la Magereza Nchini Namibia kufuatia kustaafu kwake kwa
mujibu wa Sheria. Sherehe hizo zimefanyika Februari 01, 2014 katika Chuo
cha Maafisa Magereza Mahoto kilichopo nje kidogo ya Mji Mkuu wa
Windhoek, Namibia.
![image_1](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_uCvIyU4ZdYv8QqqWHOYpYomVzhJuC3YZfJDKFVBCpc0xR3zeww2pM5fFpMCmv4CNkJ557vDu0Im44mmfn-Ma0AIe9jSXylJmFNcsJFTB5evpy8MK4e-8uuLMDjgHMTlFXXPaIgQxKV5U4=s0-d)
Baadhi
ya Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama wakiwa wamesimama kabla ya
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Evaristus Shikongo kupita
akiwa kwenye gari Maalum la Wazi wakati akiwapungia mikono Maafisa,
Askari pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Namibia ikiwa ishara
ya kuwaaga rasmi kufuatia kustaafu kwake Utumishi wa Umma akiwa
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Namibia tangu mwaka1995. Wa kwanza
kulia ni Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania, John Casmir
Minja(wa pili kulia) ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini Namibia, Luteni
Jenerali John Mutwa(wa tatu kulia) ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini
Namibia, Inspekta Jenerali wa Polisi Denga Ndaitunga(wa tatu kulia) ni
Mkuu wa Majeshi Mstaafu Nchini Namibia, Lueni Jenerali Mstaafu Martin
Chalinde( wa pili kulia).
Kamishna
Jenerali wa Magereza Nchini Namibia, Evaristus Shikongo akiwa kwenye
gari Maalum la Wazi huku akiwapungia mikono baadhi ya Maafisa na Askari
wa Magereza Nchini Namibia katika sherehe za kukabidhi Madaraka ya
Uongozi wa Magereza Nchini Namibia Februari 01, 2014 ambapo sherehe hizo
zimefanyikia katika Chuo cha Maafisa Magereza wa Namibia kilichopo nje
kidogo ya Mji Mkuu wa Windhoek, Namibia. ![image_3](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_sQ50YNNAUDy9fibguU-i1L2SvT_X_li7bFRqchV60VmLn2b0jiLsm3j7W6E1AZCF7-ALYlrPyasTPaMtawC-a_tUrF8vc5kN0997jNmeFFkZw5HgtQXDm1bck-Ca7tkvBE1bN2fpMXfqs=s0-d)
Gadi
iliyounda Gwaride Maalum ya Wanawake, Maafisa wa Jeshi la Magereza
Nchini Namibia wakipita mbele ya Mgeni rasmi huku wakiwa katika Mwendo
wa haraka kama wanavyoonekana wakiwa kikakamavu Februari 01, 2014 katika
Sherehe za Makabidhiano ya Uongozi wa Jeshi la Magereza kufuatia
kustaafu rasmi Utumishi wa Umma kwa Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini
Namibia, Evaristus Shikongo( hayupo pichani). ![image_4](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_u8B-gy1ZmuhIjWXFqJRxdCODtG3ZHipO2EkjbFaVLTEJhWFJbRU4zJGat8rNthAskqX2p5w8bC7kUlh0rnPPKarB1Ps66YJSlWGCRbIsMn1xLZ0Dn5X-8w5oacO61IGV9AAeXyiatsDA=s0-d)
Kamishna
Jenerali wa Magereza Nchini Tanzania, John Casmir Minja(kushoto)
akimpongeza Kamishna Jenerali Mstaafu wa Magereza Nchini Namibia,
Evaristus Shikongo(kulia) mara baada ya kukabidhi rasmi Madaraka ya
Uongozi wa Jeshi la Magereza Nchini Namibia Februari 01, 2014 katika
Sherehe zilizofana sana nje kidogo ya Mji Mkuu wa Windhoek, Namibia(
Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza). ![photo](https://lh3.googleusercontent.com/blogger_img_proxy/AEn0k_vCOJYadO-qLe2LyBecDwAJMBascgeZlQem3GFXn52pelbtg7cFifjS5ZlnsmoLq7LUyDvXxNVnDdcVtErv4Se2Kjsr6o8E4GuZmUJeDHj_NB2nsT1VtxecE9GN3nbTB767sfz8DeaV=s0-d)
Kamishna
Jenerali wa Magereza Nchini Namibia anayemaliza muda wake, Evaristus
Shikongo(katikati) akipokea Salaamu ya heshima toka kwa Gwaride Maalum
lililoandaliwa na Maafisa na Askari wa Magereza wa Namibia(hawapo
pichani) wakati wa sherehe za kukabidhi rasmi Uongozi(kulia) ni Waziri
wa Ulinzi na Usalama Nchini Namibia, Mhe. Immanuel Ngatjizeko na kushoto
kwake ni Kamishna Jenerali Mpya wa Magereza Nchini Namibia, Raphael
Hamunyela. Sherehe hizo zimefanyika Februari 01, 2014 katika Chuo cha
Maafisa Magereza Mahoto kilichopo nje kidogo ya Mji Mkuu wa Windhoek,
Namibia.
Post a Comment