SERIKALI imeonya kuwa, mashine za kielektroniki (EFD) zisiwe chanzo cha kuvuruga amani ya nchi, na zitaendelea kutumika kwa mujibu wa sheria.
Imesema msimamo wake uko pale pale na kamwe hautabadilika.
Kwa mujibu wa serikali, hakuna sababu ya kuendelezwa mjadala huo, kikubwa ni wafanyabiashara kufuata sheria za nchi.
Waziri wa
Fedha, Saada Mkuya Salum, akizungumza kwa simu jana, alisema msimamo wa
serikali ni kwamba mashine zitaendelea kutumika.
Alisema
wataendelea kuwaelimisha wananchi kuhusu matumizi ya mashine hizo na
kwamba, elimu imeshatolewa kwa wafanyabiashara wengi.
“Mashine hizi zipo kisheria, zitaendelea kutumika na tunaomba zisiwe sababu ya kuleta mtafaruku, kuvuruga nchi na kuhatarisha amani,” alisema.
Saada alisema
kabla ya kuanza matumizi ya mashine hizo, elimu ilitolewa kwa
wafanyabiashara kuhusu umuhimu wake na inaendelea kutolewa, hivyo
wanaozipinga ni kwa utashi wao.
Waziri alisema
madai mengi ya wafanyabiashara kuhusu matumizi ya mashine hizo
yameshafanyiwa kazi, hivyo kuwataka kuendelea kuzitumia kama sheria
ilivyoelekeza.
Kwa mujibu wa Saada, baadhi ya watu waache wamekuwa wakiwashawishi wafanyabiashara kuhusu matumizi ya mashine hizo.
Kwa takriban siku tatu baadhi ya wafanyabiashara wameingia kwenye mgomo wa kutokufanya biashara wakigomea matumizi ya EFD.
Wafanyabiashara
hao, wakiwemo wa maduka eneo la Kariakoo, Dar es Salaam na baadhi ya
mikoa, wanapinga matumizi ya mashine hizo, wakiitaka serikali
kubadilisha mfumo huo wa ukusanyaji mapato.
>>Uhuru
>>Uhuru
Post a Comment