Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TUZO ZA MUZIKI TANZANIA KTMA 2014 ZAZINDULIWA RASMI LEO


Kilimanjaro Tanzania Music Awards (KTMA2014), ni tuzo ambazo hufanyika kila mwaka kwa lengo la kutambua kazi bora za wasanii ambazo zimefanya vizuri ndani ya mwaka mzima. Mapema hii leo, Meneja wa bia ya Kilimanjaro, Bwana George Kavishe alifungua tuzo hizo rasmi na kutoa maelezo kwa mabadiliko ambayo yamejitokeza mwaka huu…

Baadhi ya mabadiliko ambayo yataonekana safari hii, ni kwa mara ya kwanza mashabiki watakuwa na nafasi ya kupendekeza kwa njia ya SMS, barua pepe na kupitia tovuti jina la msanii, kikundi au mtayarishaji wa Muziki aliefanya vizuri.
Pia, kwenye tuzo za mwaka huu, vipengele vitakavyopigiwa kura vitakuwa 34.
 

Kampuni ya bia ya Tanzania (TBL) kwa ushirikiano na Baraza la Sanaa Tanzania  (BASATA) leo tumezindua rasmi msimu mwingine wa Tuzo za Muziki Tanzania  zinazojulikana kama KTMA.


Mkutano na wana habari za michezo na burudani kutoka vyombo mbali mbali ndio umezindua msimu huu katika hoteli ya Kebby’s ilioko maeneo ya Mwenge  jijini Dar es Salaam. Viongozi wa BASATA pamoja na wa bia ya Kilimanjaro walizungumzia mabadiliko chanya katika mchakato wa mwaka huu ikiwa ni 
juhudi na hatua za kuendelea kuboresha mfumo wa upatikanaji wa wateule  wa vipengele mbali mbali vya tuzo hizi.

Mabadiliko:
Mwaka huu watanzania wamepewa fursa ya kupendekeza wasanii, nyimbo, vikundi,  watayarishaji, video n.k wanazodhani zinastahili kuwepo kwenye mchakato  wa kuwapata wateule wa tuzo za muziki Tanzania. Kwakutumia mfumo wa SMS  na mtandao wapenzi wa muziki wataweza kutoa mapendekezo yao kupitia;

a. Namba ya simu 15440.
b. Mtandao – Website/tovuti na barua pepe/email.


Semina fupi ilioendeshwa katika hoteli ya Kebbys ilitoa ufafanuzi wa jinsi ya 
kutoa mapendekezo na wapi mpenzi wa muziki anaweza kwenda kupata maelezo ya ziada yanayohusiana na njia za kutumia kupendekeza kazi na wasanii  wanaowataka.

“Baada ya tathmini ya mwaka jana, tumeonelea wakati wa kuwahusisha wapenzi wa  muziki umewadia. Tuzo za muziki ni mchakato endelevu unaoendelea kubadilika kila mwaka ikiwa ni jitihada za kuboresha na kuhakikisha  mfumo unakua imara, kuhakikisha tunapata wateule na washindi  wanaostahili’. Alisema George Kavishe meneja wa bia ya Kilimanjaro.


‘Kama una amini msanii unaempenda ama kikundi ama wimbo n.k inastahili  kuingizwa kwenye mchakato, basi pendekeza.’ Alisema George.


BASATA waliwapongeza TBL kwa kuendelea kuwa wabunifu na kuwa makini na  tathmini pamoja na taarifa mrejesho (feedback) za wapenzi wa muziki na  kuendelea kuzifanyia kazi alimradi kuboresha mfumo mzima wa tuzo hizi za  kitaifa. 

“BASATA ilipewa nafasi ya kutathmini mchakato huu mpya na tumeuridhia na  kuonelea ni mfumo mzuri wenye tija na utakaoleta matoke mazuri zaidi kwa mchakato wa tuzo hizi.” Alisema mwakilishi wa BASATA.

Taarifa kamili za njia ya kupendekeza zipo kwenye mtandao wa Kili http://www.kilitime.co.tz/ktma pamoja na page ya facebook ya Kilimanjaro na kwa taarifa unaweza kuifata handle ya kili @kilimanjarolarger kwenye twitter.

Usiku wa tuzo unatazamiwa kuwa ni tarehe 3-Mei-2014 katika ukumbi wa Mlimani City.


Kwa taarifa zaidi wasiliana na wasimamizi wa taarifa na mchakato wa KTMA,  1Plus kupitia anuani ilioainishwa hapo chini au na George Kavishe, 
meneja wa Kilimanjaro. 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top