Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

DIWANI NA AFISA MTENDAJI WANUSURIKA KUCHOMWA MOTO HUKO IGUNGA


 
Diwani wa Isakamaliwa, Igunga, Doto Kwilasa, Ofisa Mtendaji wa Kijiji, Erasto Shokoro, wajumbe sita wa serikali ya kijiji na mtu ambaye hajajulikana wamenusurika kuchomwa moto na wananchi.
 
Wananchi hao waliwafungia ndani ya chumba cha mikutano viongozi hao kwa madai ya kuitisha kikao cha kuwazuia vijana wa Isakamaliwa wasilipize kisasi kwa wafugaji waliowachoma mikuki vijana wenzao.
 
Vurugu za kutaka kuchoma moto chumba hicho zilitokea juzi katika Kijiji cha Isakamaliwa baada ya makundi mawili ya wafugaji wa kata hiyo kutofautiana na kusababisha kundi moja kushambulia jingine kwa mikuki wakidaiwa kuingiza mifugo kinyume cha sheria katika bonde la Magogo.
 
Chanzo;Tanzania Daima
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top