Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AMNADI RIDHIWANI KIKWETE KATIKA MVUA KUBWA

3


2Mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi Ndugu Ridhiwani Kikwete akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Ubena Zomozi katika mkutano wa kampeni uliofanyika  kijijini hapo huku mvua kubwa ikinyesha na kuwafanya wananchi hao kugeuza viti vyao na kuvifanya miamvuli ya kujikinga na mvua hiyo, kutokana na kukunwa na hotuba ya mgombea ubunge huyo ambaye alizungumzia matatizo mbalimbali yakiwemo masuala ya maji, umeme, elimu afya na mengine kadhaa na kuahidi kuyafanyia kazi na kuyatekeleza kwa kufuata ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi CCM, Uchaguzi wa jimbo la Chalinze unafanyika Aprili 6 jumapili kuziba pengo la aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Saidi Bwanamdogo aliyefariki dunia hivi karibuni6Baadhi ya wananchi wakiwa wamejikinga na mvua kwa kutumia viti vyao
5Baadhi ya wananchi wakiwa wamejikinga na mvua kwa kutumia viti vyao wakati wakifuatilia hotuba ya Ridhiwani Kikwete alipowaomba kura katika kijiji cha Ubena Zomozi leo.4Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wa pili kutoka kulia pamoja na viongozi wa kijiji hicho wakifuatilia hotuba ya mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete huku wakiwa wamesimama kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha wakati wa mkutano huo.
3Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimuombea kura Ridhiwani Kikwete huku mvua ikinyesha ambapo aliwaambia wananchi hao wamchague mgombea huyo kwakuwa Chama cha Mapinduzi kimemuamini na kumsimamisha katika kuomba nafasi hiyo na kinaamini kwamba anatosha.8Umati wa tu ukiwa katika mkutano huo kabla ya mvua kunyesha.9Kikundi cha ngoma kikitumuiza katika mkutano huo.10Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Ridhiwani Kikwete wakati walipokuwa wakiwasili katika eneo la mkutano kulia ni Mzee Kazidi Meneja kampeni wa mgombea huyo ambaye pia ni Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro.11Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati Ridhiwani Kikwete kulia nia Mwenyekiti wa kata ya Fukayose Olinjurie Marigwa  wakiwasili katika eneo la mkutano Ubena Zomozi.13Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Dr. Shukuru Kawambwa mbunge wa jimbo la Bagamoyo na Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi katikati ni Mwenyekiti wa tawi la Msolwa Khalfan Changali. 14Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Ridhiwani Kikwete wakati mkutano huo wa kampeni ulipokuwa ukiendelea.15Dr. Shukuru Kawambwa mbunge wa jimbo la Bagamoyo na Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi akimuombea kura Ridhiwani Kikwete16Joseph Msukuma Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita akimuombea kura Ridhiwani Kikwete.
.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-CHALINZE)
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top