Suarez akifunga bao lake la 29 katika ligi kwa msimu huu wakiizamisha Spurs kwa 4-0 |
VIJOGOO wa
Anfield, Liverpool imekwea hadi kileleni mwa Ligi Kuu ya England
wakiiporomosha Chelsea baada ya kuifumua bila huruma Tottenham Hotspur
iliwatembelea kwenye uwanja wao.
Liverpool iliitambia vijogoo wenzao wa
London kwa kuwakandika mabao 4-0, na kuwafanya wafikishe jumla ya pointi
71, mbili zaidi ya Chelsea ambao jana walifumuliwa bao 1-0 na Crystal
Palace.
Wageni walianza kujitabiria janga baada ya
Younes Kaboul kujifunga dakika ya pili ya mchezo kabla ya Luis Suarez
kuandika bao la pili dakika ya 25 na wenhyeji kwenda mapumziko wakiwa
mbele kwa bao 2-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa Liverpool
kuandika bao la tatu kupitia kwa Phillipe Countinho dakika ya 55 kabla
ya Jordan Henderson katika dakika ya 75 na kuifanya Liverpool kukalia
kiti cha uongozi kilaini.
Post a Comment