Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

‘Makahaba’ wavamia Dom

 
“‘Short time’ vipi? Ni Sh.10,000 tu, gharama ya chumba kwangu.” Hivi ndivyo nilivyopokelewa na binti wa miaka 21 katika Mtaa wa Uhindini mkoani Dodoma nilikokwenda saa 4 usiku kufuatilia taarifa za kinadada wanaofanya biashara haramu ya ngono, maarufu kama changudoa.
Uhindini ni mtaa maarufu mkoani Dodoma kwa biashara ya ngono, ikifuatiwa na maeneo mengine kama Chako ni Chako, Mwanga Bar na zaidi, katika kumbi za starehe kama Club 84 na Maisha.

Wakati nazungumza na binti huyo mfupi na maji ya kunde, kinadada wengine kadhaa, walikuwa wakitufuatilia kwa karibu kuona kama tumekubaliana au tumeshindwana bei ili na wao wataje gharama zao.
“Sh.8,000 huduma ya chapchap (short time) chumbani, Sh.5000 hapa hapa na Sh.70,000 saa 5:00 (usiku) mpaka asubuhi,” walijinadi wengine wakijaribu kile wanachokiita bahati yao.
Hata hivyo, baada ya kugundua kuwa sikuwa na lengo la kufanya nao biashara, wote walirudi nyuma kusubiri wateja wengine. Ndipo nilipomwita binti huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Monica na kufanya naye mazungumzo kama ifuatavyo;
Mwananchi: Habari yako binti? Mimi niko hapa kikazi na ningeomba nichukue dakika zako kadhaa ambazo nitazilipia kwa Sh.10,000. Nilitamani kujua kazi hiyo ulianza lini na nini kilikusukuma kuifanya?
Monica: Ni hadithi ndefu. Nilianza kuifanya mwaka juzi nikiwa na umri wa miaka 19. Nililazimika kuifanya baada ya baba yangu wa kambo kuonyesha kutokunijali kabisa na nikahisi sina thamani kwenye familia yake.
Mwananchi: Wewe ni mwenyeji wa wapi na wateja wako ni kina nani hasa?
Monica: Mimi ni mtu wa Singida, naifanya biashara hiyo sanasana hapa Dodoma wakati wa Bunge. Baada ya hapo narudi kuendelea nayo huko huko Singida.
Mwananchi: Unatumia vigezo gani kupanga gharama za huduma zako?
Monica: Inategemea nazungumza na mtu mwenye mwonekano gani. Gharama ya short time kwa mtu wa hali ya juu inaanzia Sh.20,000 na kulala ni Sh.100,000 hapa malipo ya chumba kwangu. Kwa mtu wa kawaida naanzia Sh.5000 short time hadi Sh.20,000 hii hakuna kulala.
Mama mtu mzima anayekadiriwa kuwa na kati ya umri wa miaka 40 na 50 ambaye hakutaka kutaja jina lake, anaeleza kuwa biashara ya ngono imemsaidia katika mambo mengi, ikiwamo kuwasomesha watoto wake wawili; mmoja chuo kikuu na mwingine kidato cha nne.
 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top