Na Gladness Mushi, Arusha
Mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela ametoa wito kwa makampuni
ya hisa hapa nchini kuhakikisha kuwa yanajiwekea utaratibu wa kutoa
elimu kwa watanzania juu ya umuhimu wa kuweka na kununua hisa kwani
takwimu bado zinaonesha kuwa asilimia kuwa ya watanzania bado uelewa wao
upo chini sana.
Mongela aliaysema hayo wakati
akiongea na wajasiriamali pamoja na wadau wa mfuko wa soko la hisa la
Dar es saalam DSE mapema jana jijini Arusha.
Alibainisha kuwa kwa sasa masoko
ya hisa ni mengi sana lakini asilimia kubwa ya watanzania bado
hawajaweza kuwa na uelewa wa kutosha juu ya umuhimu wake hali ambayo
inatakuiwa itatuliwe tena kwa haraka sana.
Katika hatua nyingine Mongela alidkuwa ili uchumi wa nchi ya Tanzania uweze kukua ni lazima hata wajasirimali nao waweze kubebwa kwa kupewa elimu sanjari na mbinu za kuwafikisha katika malengo yao mbalimbali.
“kama tukiwawekea utaratibu mzuri hawa wajasiriamali lakini pia
wafanyabiashara wadogo basi mitaji itaongezeka na wataweza kujiendesha
wao wenyewe na hivyo uchumi wa nchi nao utaweza kuimarika kwani uwezo
huo upo kabisa”aliongeza Mongela.
wafanyabiashara wadogo basi mitaji itaongezeka na wataweza kujiendesha
wao wenyewe na hivyo uchumi wa nchi nao utaweza kuimarika kwani uwezo
huo upo kabisa”aliongeza Mongela.
Naye Mwanasheria wa soko hilo la hisa la Dar es saalam. Mary Muniwasa
alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa wafanyabishara wadogo na wa
daraja la kati wameanzisha rasmi dirisha la kukuza ujasiriamali kwa
malengo ya kuboresha uchumi wa nchi.
alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa wafanyabishara wadogo na wa
daraja la kati wameanzisha rasmi dirisha la kukuza ujasiriamali kwa
malengo ya kuboresha uchumi wa nchi.
aliwataka wafanya biashara wote hapa nchini kuhakikisha kuwa wanatumia
vema dirisha hilo la kukuza ujasiriamali kwa maslahi ya kuboresha
uchumi na maendeleo ya Nchi ya Tanzania.
vema dirisha hilo la kukuza ujasiriamali kwa maslahi ya kuboresha
uchumi na maendeleo ya Nchi ya Tanzania.


Post a Comment