Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ujumbe kwa Diamond, fanya haya ufikie utajiri wa Jay-z

Jay-z ana utajiri unaokadiriwa dola millioni 475 za kimarekani kwa takwimu za mwaka 2013. Mafanikio ya jay-z yamefikiwa kwa kiasi kikubwa kwa biashara anazofanya.Kufanya zaidi, Kujitoa zaidi na kuona zaidi  ndio kinachomfanya jay-z azidi kusimama kama nguli hatari wa muziki, fashion excecutive na mkali wa burudani. Ukiongelea Jay-z kama Jay-z basi unaweza kutumia mstari kutoka kwenye nyimbo ya kanye west “Diamonds From Sierra Leone”: “I’m not a businessman, I’m a business, man!”  yaani ikimaanisha yeye sio mfanyabiashara bali yeye mwenyewe ndio biashara. Hiki ndio kitu kilichokosekana hapa bongo, msanii kubadilisha mtazamo wake kama anafanya biashara na kuanza kuji-brand  mwenyewe kama biashara. Hivi sasa Diamond ndio msanii pekee ambayo anaweza kubadilisha vitu kadhaa na kufika level alizopo Jay-z na hivi ndivyo vitu vya kufanya ;-
Diamond-na-jay-z-ofisini
Kua mtafutaji zaidi
Kabla  Shawn Carter ajawa  Jay-Z, akiwa na miaka 12 alikua akiuza madawa ya kulevya maeneo ya  Marcy Projects , maeneo hatari sana huko Brooklyn. Japokua jay-z hakuwa anafanya kitu kizuri lakini ule moyo wa
kutafuta ndio umemfanya afike alipo sasa. Japokua Diamond ana historia kidogo kama jay-z sababu naye mwaka 2008 na 2009 alikuwa akifanya kazi katika kiwanda cha mabegi kilichoko Mikocheni na kulipwa mashahara wa shilingi 2,000 kwa masaa 8, huku nauli ikimgharimu shilingi 1,000 mpaka kufika kwao na hapo chakula ni zaidi ya shilingi 1,000.Ameshauza maji hadi mitumba . Somo ambalo amejifunza jay-z  akifanya biashara mtaani ni kutompa mtu discount , kama aliuza kitu kwa dola 10 basi hawezi kupunguza iwe dola 9.95 hata kama ni rafiki yake wa karibu. Hiki ni kitu kinachowafanya wasanii wengi wasifanikiwe hasa wasanii wakubwa. Katika kitabu chake cha decoded jay-z alisema “Nilioamua kujiingiza katika rap, sikuwa nimeweka kiapo cha umaskini,niliona ni nafasi nyingine ya kupigana, nafasi ambayo inaendana na kipaji changu halisi cha muziki.nilikua msanii mwenye hamu na mwenye kusita pia,lakini umuhimu wa ninachotaka kufanya ndio ulisababisha mambo yote yafanikiwe, inabidi uwe msanii usiyebadilika”
Diamond-Jay-z-Performing
Kutengeneza opportunity zako mwenyewe
Kwa jay-z mafanikio hayakua tu kuchukua opportunities zilizokwepo, ilikua ni kutengeneza opportunity zake mwenyewe. Jay-z alipoanza kurap kulikua hakuna label ambazo zilikua tayari kumchukua kwahiyo akaamua kushirikiana na  Damon Dash and Kareem Burke kutengeneza label yake mwenyewe ya , Roc-A-Fella Records. Inashangaza kwa mafanikio aliyonayo diamond kwasasa ameshindwa hata kuanzisha recoring label yake mwenyewe na kutegemea kila siku kusumbuka kwenye label za watu wengine. Jay-z pia alikua ni mpenzi wa fashion hasa brand ya  Iceberg Apparel ya italia aliamua kushirikiana na Dash na kuanzisha brand ya nguo za  Rocawear, ambayo aliiuza baadae kwa $204 million. Diamond sasa ameanza biashara ya nguo lakini inaonekana kutovutia watu wengi so inabidi ajipange kuja na brand moja hatari.
Biashara-Diamond-Jay-z
Kuwa power couples
Jay-z na beyonce ndio celebrity couples wanaoongoza kuingiza pesa nyingi duniani kutokana na takwimu zilizofanywa na forbes. Kama tunavyojua unaweza kujiita mwenye bahati kama utaweza kuspend siku nzima ofisini na partner wako bila ya kurushiana stepler. lakini Beyonce na Jay-z  wanaweza kujihesabia kama wenye bahati kwasababu wameweza kufanya kazi pamoja na kuwaingizia dola za kimarekani millioni 95 mwaka jana. Wema Sepetu na Diamond Platnumz ndiyo super couples pekee iliyopo bongo, tumeona wakituonesha malavidavi lakini katika maswala serious ya kuingiza mshiko hawajaweza kutumia kigezo hicho kujitajirisha.Sasa ni wakati muafaka wa diamond kutulia na wema sepetu na kuangalia watatumiaje umaarufu wao kuingiza mshiko kama wanavyofanya jay-z na beyonce .
Super-couples-jay-z-beyonce-Diamond-Platnumz-Wema-Sepetu

vibe

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top