Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ATUPWA JELA KWA KOSA LA KUMCHANJA MKEWE KWA KISU


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Nkasi imemtia hatiani mkazi wa kijiji cha Kabwe Camp mwambao mwa Ziwa Tanganyika, Halid Mussa (38) kwa kosa la kumjeruhi mkewe, Mwajuma Idd(23) kwa kumchanja viganja vyake na kifuani kwa kisu kwa kile kilichodaiwa wivu wa kimapenzi.

Mshtakiwa huyo ambaye alihukumiwa jana na Hakimu wa Mahakama hiyo, Ramadhan Rugemalira ameanza kutumikia kifungo cha miezi sita baada ya kushindwa kulipa faini ya Sh 100,000.

Akitoa hukumu hiyo, Rugemalira alidai mahakamani hapo kuwa upande wa mashtaka ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Hamimu Gwelo umeithibitishia mahakama hiyo kuwa mshtakiwa kweli alitenda kosa hilo. Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Desemba 27, mwaka jana usiku wa manane nyumbani kwake Kabwe Camp.

Ilidaiwa mahakamani hapo usiku huo wa tukio mshtakiwa akiwa na rafiki yake aitwae Mhaya walikuwa wakinywa pombe ya kienyeji katika klabu moja iliyokuwa ikiuza kilevi hicho kijijini humo ambapo rafiki yake huyo alimuaga akidai kuwa ametosheka kunywa pombe.

Kwa mujibu wa Hakimu, Rugemalira mshtakiwa naye aliamua kurejea nyumbani kwake na alipoingia ndani alipishana na rafiki yake huyo akitoka chumbani alimolala mkewe.

Akijitetea mahakamani hapo mshtakiwa aliiomba mahakama hiyo impunguzie adhabu kwa kuwa anatunza watoto watano alioachiwa na marehemu mkewe wa kwanza.

Hata hivyo Mwendesha Mashitaka, Gwelo aliiomba mahakama hiyo itoe adhabu kali kwa mashtakiwa ili iwe fundisho kwake na wengine wenye tabia ya kunyanyasa wanawake ambapo sasa tabia hiyo imekuwa tatizo.
NA PETI SIYAME
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top