Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAHAMIAJI HARAMU 47 WATIWA MBARONI MKOANI KILIMANJARO

 

IDARA ya Uhamiaji  kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi , mkoani Kilimanjaro, inawashikilia wahamiaji haramu 47 raia wa Ethiopia, kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria. Mbali na wahamiaji hao, Idara hiyo inamshikilia Mtanzania mmoja Benjamini Saimon (28) mkazi wa Kibamba, Dar es salam, kwa tuhuma za kuhusika na kuwasafirisha wahamiaji hao.
Akiongea na FIKRAPEVU Ijumaa, Aprili 4, mwaka huu, Mkuu wa Uhamiaji mkoa wa Kilimanjaro, Johannes Msumule, alisema wahamiaji hao walikamatwa Alhamisi ya April 3, mwaka huu,  saa 9:30 usiku katika eneo la Chekereni katika kata ya Kahe Wilaya ya Moshi barabara kuu ya kutoka Moshi kwendaTanga.
Amesema raia hao wa Ethiopia, walikamatwa wakiwa kwenye gari aina ya Mitsubish Fuso lenye namna za usajili T216 ASU wakidaiwa kujiandaa kwenda Afrika Kusini. 
“Mwezi wa tano tunaenda katika maeneo ya mipakani kutoa elimu kwa wananchi wanaoishi kule, kama Kilobo, Kileo, Holili, Kifaru na maeneo yote ili tuweze kufanya hii kazi kwa kushirikiana na wao” alisema Msumule.
Hata hivyo, alisema kwa sasa idara hiyo imejipanga vizuri ili kuweza kutokomeza tatizo la wahamiaji haramu, ambao kwa sasa wameanza kufuatilia ili kuwabaini watu ambao wamekuwa wakijihusisha na kazi ya kuwasafirisha. Alisema katika kipindi cha miezi mitatu ya mwaka huu, jumla ya wahamiaji haramu 216 wamekamatwa katika maeneo mbalimbali nchini. 
Alisema jumla ya Kesi 12 zimefikishwa mahakamani ambapo kesi moja imemalizika na nyingine 11 bado zinaendelea.
- See more at: http://www.fikrapevu.com/wahamiaji-47-toka-ethiopia-watiwa-mbaroni-kilimanjaro/#sthash.6GKgFTpC.dpuf
IDARA ya Uhamiaji  kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, mkoani Kilimanjaro, inawashikilia wahamiaji haramu 47 raia wa Ethiopia, kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria. Mbali na wahamiaji hao, Idara hiyo inamshikilia Mtanzania mmoja Benjamini Saimon (28) mkazi wa Kibamba, Dar es salam, kwa tuhuma za kuhusika na kuwasafirisha wahamiaji hao.  
Akiongea, Mkuu wa Uhamiaji mkoa wa Kilimanjaro, Johannes Msumule, alisema wahamiaji hao walikamatwa Alhamisi ya April 3, mwaka huu,  saa 9:30 usiku katika eneo la Chekereni katika kata ya Kahe Wilaya ya Moshi barabara kuu ya kutoka Moshi kwendaTanga.  
Amesema raia hao wa Ethiopia, walikamatwa wakiwa kwenye gari aina ya Mitsubish Fuso lenye namna za usajili T216 ASU wakidaiwa kujiandaa kwenda Afrika Kusini.
“Mwezi wa tano tunaenda katika maeneo ya mipakani kutoa elimu kwa wananchi wanaoishi kule, kama Kilobo, Kileo, Holili, Kifaru na maeneo yote ili tuweze kufanya hii kazi kwa kushirikiana na wao” alisema Msumule.  
Hata hivyo, alisema kwa sasa idara hiyo imejipanga vizuri ili kuweza kutokomeza tatizo la wahamiaji haramu, ambao kwa sasa wameanza kufuatilia ili kuwabaini watu ambao wamekuwa wakijihusisha na kazi ya kuwasafirisha. 
Alisema katika kipindi cha miezi mitatu ya mwaka huu, jumla ya wahamiaji haramu 216 wamekamatwa katika maeneo mbalimbali nchini.   
Alisema jumla ya Kesi 12 zimefikishwa mahakamani ambapo kesi moja imemalizika na nyingine 11 bado zinaendelea. 
>>fikrapevu
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top