BREAKING NEWS!!! TANZANIAN HUMAN TRAFFICKERS BUSTED IN MACAU, CHINA [VIDEO].
Siku
ya Ijumma 4 April 2014 niliripoti kuhusu mabinti wakitanzania walioko
nchini China ambao wanatumikishwa kufanya biashara haramu ya ngono na
wanaojiita MAMA au BOSS LADY.
Baada ya kuweka audio clips za hao mabiniti wakilalamika na kuomba
msaada ndipo nilipo amua kuanzisha campaign ili kuwasaidia mabinti hao
walioko MACAU. Nilijaribu kwa hali na mali kutafuta mawasilano ili kujua
wako wapi na kama habari hizi ni za ukweli. Nilibahatika kuongea na
baadi ya watu wanao ishi huko na wakanihakikishia kwamba habari hizo ni
za kweli na walinihakikisha kwamba kuna mabinti wadogo sana wanaotumiwa
katika biashara hiyo haramu na wanahitaji msaada haraka iwezekanavyo
ingawa wanaogopa kutokana na vitisho wanavyopewa na hao wanaojiita
mabosslady au mama zao. Baada ya hapo ndipo harakati za kuwasaidia
zilipo anza na kwa kushirikaina na kaka yangu KWAME tukawasiliana na
shirkia la IOM (International Organization for Migration) ambao ndo mara
nyingi husaidia watu wenye matatizo kama haya kurudi nyumbani
wakatushauri cha kufanya so tukawasiliana na police wa MACAU na
kuwaelezea tatizo zima na ndipo jana Jumamosi 5 April 2014 walifanikisha
zoezi hilo kama inavvyo repotiwa hapa chini kwenye taarifa ya habari ya
TDM ENGLISH NEWS ya MACAU:
Natoa wito kwa Serikali kupitia wizara yake husika kuliangalia kwa
ukaribu hili suala na kuweza kuwaelimisha mabinti huko nyumbani juu ya
mambo haya na athari zake. Yaelekea wengi wanapelekwa nchi za watu bila
kuelimishwa vizuri au bila kuwa na ufahamu wa nini haswa wanaweza
kukutana nacho huko. Tuna penda kuishukuru Serikali ya Macau kupita
jeshi lake la Polisi kwa kuweza kuwafikisha katika vyombo vya sheria
wahusika wa biashara hii harua ya Human Trafficking.
Post a Comment