Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WATALII MABILIONEA WA MAREKANI WAMALIZA ZIARA SERENGETI

 

8880ca0dedL
HIFADHI ZA TAIFA TANZANIA
logo-tanapa
TAARIFA KWA UMMA
Watalii Mabilionea 42 kutoka Marekani wamemaliza  ziara yao ya utalii ya siku nne katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuelezea kufurahishwa kwao na uzuri wa hifadhi pamoja na maajabu ya wanyama mbalimbali wanaopatikana Serengeti ikiwemo msafara maarufu wa wanyama wahamao aina ya nyumbu.
Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alipata fursa ya kuwaaga watalii hao walipokuwa wakiondoka nchini kuendelea na ziara ya utalii katika nchi nyingine za Afrika wakitumia ndege binafsi aina ya Boeing BBJ 737 HB-11Q inayomilikiwa na Kampuni ya Utalii ya Abercrombie  & Kent ya nchini Marekani.

Watalii hao walioingia nchini Machi 28, mwaka huu wakiongozwa na Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Kampuni ya Abercombie & Kent, Geoffrey Kent wameelekea katika nchi za Italia, Botswana, Malawi, Zambia, Uganda, Namibia, Ethiopia na Afrika Kusini ikiwa ni muendelezo wa ziara yao ya kitalii katika nchi za Afrika.
Hili ni kundi la pili likifuatia ziara iliyofanywa na kundi jingine la mabilionea waliotembelea Serengeti mapema mwezi wa tatu mwaka huu kwa siku tatu na makundi yote yalifuatana na wanahabari kutoka kituo cha Televisheni cha Marekani cha CNBC ambao wamekuwa wakichukua picha na matukio mablimbali ya ziara hiyo kwa ajili ya kurusha katika kituo hicho kupitia kipindi chao maarufu kinachofahamika kama “Secret Lives of the Super Rich.”
Kipindi hiki hurushwa kupitia kituo hiki katika mataifa ya Marekani, Asia, Ulaya, Mashariki ya Mbali na Afrika.
Kwa upande wake Waziri Nyalandu alisema ujio wa watalii hao matajiri ni faraja kwa sekta ya utalii kwa kuwa itajenga imani kwa wenzao ambao hawajafika nchini kutembelea vivutio vya utalii.
Hivi sasa sekta ya utalii inachangia asilimia 17 ya Pato la Taifa na Marekani ndiyo nchi inayoongoza kwa kuleta watalii wengi nchini wanaofika kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini. Waziri Nyalandu alibainisha kuwa malengo ya wizara yake ni kuhakikisha sekta hiyo inachangia asilimia 25 ya Pato la Taifa.
Nyalandu alisema Serikali inakusudia kuhamasisha utalii wa makundi kwa kutumia ndege binafsi na mabasi kulingana na uwezo wa watalii wenyewe.
Imetolewa na Idara ya Mawasiliano
Hifadhi za Taifa Tanzania
02.04.2014
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top