Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Wazazi 100 mkoani Ruvuma wafikishwa mahakamani kwa kosa la kusherehekea watoto wao kefeli mitihani




Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu ameiambia kuwa Serikali ya Mkoa huo imewafikisha mahakamani wazazi 100 kwa tuhuma za kufanya sherehe baada ya watoto wao kufeli mitihani.
Pamona na wazazi/walezi hao kujitetea kuwa walikosa karo ya kuwapeleka watoto hao shule, imeelezwa pia kuwa mazingira duni ya kufundishia na kujifunza katika Wilaya ya Tunduru,  yameelezwa ni moja ya sababu inayowafanya wazazi kushawishi watoto wasisome kwa bidii wala kufaulu mitihani, ambapo mwanafunzi akifeli mtihani wa darasa la saba hufanyiwa sherehe.

Imeelezwa pia kuwa wanafunzi wanaosoma katika Shule za msingi Wilayani Tunduru mkoani humo huambiwa na wazazi wao kuwa wasijaze majibu yaliyo sahihi wanapofanya mitihani, bali wajaze ‘makorokocho’ ambapo kila anayefeli mtihani huo hufanyiwa sherehe na Wazazi wake.
 
Hali  hiyo  imeelezwa kuchangia kuifanya Wilaya hiyo kuwa ya mwisho Kimkoa na Kitaifa katika matokeo ya darasa la Saba mwaka jana.
 Hali ya Mkoa huo kielimu nayo hairidhishi kutokana na kuchangiwa kwa mwamko mdogo uliopo kwa wazazi na walezi. 
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top