Mchungaji Mary Izengo.
MARY Izengo (52), mkazi wa Kijiji cha Umanda- Msalala, Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza anateseka kiasi cha kutamani afe kufuatia gonjwa la ajabu alilonalo huku akisema ndugu, wakiwemo watoto wake wamemtenga.
Akizungumza
na Uwazi mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Wadi Namba 23, Jengo la
Sewa Haji kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili, mwanamke huyo alisema
usiombe gonjwa hilo likupate kwani ugonjwa unaomkabili ni wa uvimbe
mkubwa usoni ambapo unamtesa kwa kipindi kirefu huku akionekana kero
kubwa katika jamii.
Post a Comment