MKURUGENZI
wa zamani wa Shirika la Umeme nchini, (Tanesco) William Geofrey Mhando
na mamsap wake, Eva Stephem Mhando, na maofisa wengine watatu wa shirika
hilo, France Lucas Mcharange, Sophia Athanas Misidai na Naftali Luhwano
Kisinga, leo wamepandishwa kizimbani Mahakama ya Kisutu jijini Dar es
Salaam kwa kosa la kuhujumu uchumi na kuiingizia serikali hasara ya
zaidi ya shilingi milioni 884,550,000.
Katika
kesi hiyo iliyosomwa na Wakili wa Serikali, Leonard Swai, mbele ya
Hakimu Frank Mushi, wakili huyo alisema Mhando akiwa Mkurugenzi Mtendaji
wa Tanesco anatuhumiwa kumpa tenda mamsap wake ya kusambaza vifaa vya
stationery vyenye thamani ya shilingi milioni 884,550,000/ kwa shirika
hilo kinyume na taratibu.
(PICHA : RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY/GPL)


Post a Comment