Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SHULE YA MWALIMU NYERERE YAVAMIWA NA KUNGUNI



Baadhi ya majengo ya Shule ya Sekondari ya Pugu yakiwa katika hali ya uchakavu.
    Waandishi wa GPL wakiwa shuleni hapo wakiongozwa na mwalimu mkuu msaidizi wa shule hiyo.
Kibao cha Shule ya Sekondari ya Pugu.
SHULE ya Sekondari ya Pugu, iliyopo maeneo ya Pugu jijini Dar es Salaam, ambayo inasifa kubwa nchini kwa kuwa iliwahi kufundishwa na Baba wa Taifa, hayati Julius Kambarage Nyerere,  imevamiwa na wadudu aina ya kunguni ambao wanadaiwa kuwasumbua wanafunzi wa bweni wa shule hiyo.
Akizungumza na waandishi wetu, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo, Agustino Angelo, alisema tatizo hilo limekuwepo muda mrefu na wamejitahidi kulipunguza kwa kiasi kikubwa kwa kufanya upuliziaji (fummigation) mara mbili huku naye Mstahiki Meya wa Ilala Jerry Slaa, akiahidi kulimaliza kabisa tatizo hilo katika siku za hivi karibuni.
Waandishi wetu walizungumza na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo, ambao walikiri kusumbuliwa na tatizo hilo ambalo wanadai kuwa linawakosesha amani na kuwataka viongozi wa serikali wajitokeze kutokomeza tatizo hilo ili waendelee na masomo yao vizuri.
Mbali na hayo, waandishi wetu pia walishuhudia majengo chakavu ya shule hiyo, mazingira ambayo si rafiki na heshima ya shule hiyo yenye historia kubwa nchini.
(Picha: Chande Abdallah na Denis Mtima / GPL)
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top