Afisa
Haari wa Young Africans Bw Baraka Kizuguto (kushoto) akiwa pamoja na
mshambuliaji mpya Andrey Coutinho mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege
wa JK Nyerer leo
**********
Kiungo
mshambuliaji mpya wa timu ya Young Africans SC Andrey Marcel Ferreira
Coutinho amewasili mchana wa leo jijini Dar es salaam akitokea kwao
nchini Brazil tayari kabisa kwa kuanza kazi ya kuwatumikia wana
Wanajangwani katika msimu wa 2014/2015.
Countinho
amewasili mchana kwa shirika la Ndege la Afrika Kusini (South African
Airways) akitoka jijini Sao Paul ambapo safari ya kuja Tanzania
imemkchukua takribani masaa 20 tokea katika Mji wa Berem ambapo ndipo
anapoishi>
Mara
baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa JK Nyerere, Coutinho alipokelewa
na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Bw. Mohamed Bhinda ambaye alimuongoza
kuwasilimia washabiki na waaandishi wa habari walijitokeza kumlaki.
Akiongea
na waandishi wa habari Uwanja wa Ndege Coutinho amesema anajisikia
furaha kuwa Tanzania, nchi ambayo watu wake wanapenda mpira na kikubwa
amekuja kuisaidia Yanga kufanya vizuri kwenye michuano mbalimbali mbali
itayakayowakabili.
Kuhusu
changamoto za ugeni katika Bara la Afrika, Coutinho alisema soka kwake
ni kazi, ana uzoefu baada ya kucheza pia Barani Asia hivyo hana
wasiwasi, na kwa kuwa na walimu aliwazoea anaamini kwa pamoja atafanya
vizuri.
Msafara
wa kutoka Uwanja wa ndege ulielekea makao makuu ya klabu mitaa ya
Twiga/Jangwani ambapo Coutinho aliwasilimia wapenzi, washabiki na
wanachama waliojitokeza kumpokea, kisha aliongea na katibu mkuu Bw Beno
Njovu kabla ya kwenda kupumzika.
Post a Comment