Kwa nyakati tofauti jana, kila mmoja wao alimwambia mwandishi wetu
kwamba yupo tayari kurudiana na mwenzake, hatua ambayo inaweza kuondoa
mgogoro huo ambao umefifisha taswira yao ya kiutumishi.
Akizungumza nyumbani kwake Tabata Kimanga, Dar es Salaam, Mbasha alisema
ameshamsamehe mkewe na kwamba anamsubiri muda wowote arudi nyumbani
kusuluhisha mgogoro wao. 'Nawapenda Watanzania wote wazidi kutuombea ili mimi na mke wangu
turudiane.' Mbasha alimwambia mwandishi wa gazeti la Mtanzania.
Kauli
hiyo ni sawa na ile aliyoitoa Flora wiki iliyopita pale aliposema:
'Ninawaomba Watanzania waendelee kuniombea ili niweze kushinda majaribu
haya, kilichotokea ni sehemu tu ya kupimwa imani yangu'.
Jana, Flora alirudia kauli hiyo kupitia kwa wakili wake, Addo Mwasongwe
ambaye alisema mwimbaji huyo yupo tayari kukutana na mumewe na ndugu ili
waondoe tofauti zao.
Kwa upande wake Mbasha alisema: 'Mi namwomba Flora ajishushe akubali,
aje home (nyumbani) tuyamalize na maisha yaendelee. Yeye ni mke wangu
namtaka. Kama ananipenda arudi, tuite wazazi tutatue mgogoro huu.'
Aliongeza
kuwa hakuna binadamu yeyote asiyesamehewa na kwamba
kilichotokea katika ndoa yao ni sehemu ya maisha ambayo wengi hupitia.
'Siku zote naamini tunachotakiwa ni kujenga na siyo kubomoa'¦ Flora
asing'ang'anie kwa watu arudi hapa'¦ apige hodi'¦ 'mume wangu' nimerudi
'¦na mimi nitampokea tuendelee kulea watoto.
'Alisema Mbasha
Mbasha anakabiliwa na tuhuma za kumbaka shemejiye wa miaka 17 na kesi
yake inaendelea katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala na sasa yupo nje kwa
dhamana.
*Source:Mtanzania*
Post a Comment