Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAHABUSU WAVUA NGUO NA KUBAKI UCHI KAMA NJIA YA KUHARAKISHWA KWA KESI ZAO WILAYANI GEITA

 


Katika hali isiyo ya kawaida mahabusu wa gereza la wilaya ya Geita waliofikishwa katika mahakama ya mwanzo ya nyankumbu kugoma kurudi mahabusu kwa kuvua nguo huku waking'ang'ania mlingoti wa bendera ya taifa kwa madai ya kushinikiza haki itendeke.
Mahabusu hao wamesema kuwa kila mara wamekuwa wakifikishwa mahakamani bila ya muafaka kupatikana huku wengine kesi zao zikimalizika haraka lakini hawajui kwanini wao kesi zao zinachelewa na kumtaka mkuu wa mkoa kuingilia kati suala lao ili kupatiwa ufumbuzi.

Ni malalamiko ya baadhi mahabusu hao ambao wanaona kukaa kimya kwa muda mrefu kunawafanya kutopata haki zao.

lakini ilibidi busara itumike ya kuwataka wavae nguo ili wasikilizwe kero zao.

mahabusu hao wamedai kuwa hawana nia ya kufanya fujo na kwakuwa serikali sikivu wanaomba kusaidiwa.

Katibu tawala wilaya ya Geita Gasper Kanyaita amechukua majina ya mahabusu hao ili kufatilia mafaili yao na kujua namna ya kuwasaidia.

Baada ya kubembelezwa kwa muda mrefu hatimaye mahabusu wakakubali kurudi gerezani baada ya kuahidiwa kuja kusikilizwa kero zao siku ya leo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top