Katika hali isiyo ya kawaida mahabusu wa gereza la wilaya ya Geita
waliofikishwa katika mahakama ya mwanzo ya nyankumbu kugoma kurudi
mahabusu kwa kuvua nguo huku waking'ang'ania mlingoti wa bendera ya
taifa kwa madai ya kushinikiza haki itendeke.
Mahabusu hao wamesema kuwa kila mara wamekuwa wakifikishwa mahakamani
bila ya muafaka kupatikana huku wengine kesi zao zikimalizika haraka
lakini hawajui kwanini wao kesi zao zinachelewa na kumtaka mkuu wa mkoa
kuingilia kati suala lao ili kupatiwa ufumbuzi.
Ni malalamiko ya baadhi mahabusu hao ambao wanaona kukaa kimya kwa muda mrefu kunawafanya kutopata haki zao.
lakini ilibidi busara itumike ya kuwataka wavae nguo ili wasikilizwe kero zao.
mahabusu hao wamedai kuwa hawana nia ya kufanya fujo na kwakuwa serikali sikivu wanaomba kusaidiwa.
Katibu tawala wilaya ya Geita Gasper Kanyaita amechukua majina ya mahabusu hao ili kufatilia mafaili yao na kujua namna ya kuwasaidia.
Baada ya kubembelezwa kwa muda mrefu hatimaye mahabusu wakakubali kurudi gerezani baada ya kuahidiwa kuja kusikilizwa kero zao siku ya leo.
Ni malalamiko ya baadhi mahabusu hao ambao wanaona kukaa kimya kwa muda mrefu kunawafanya kutopata haki zao.
lakini ilibidi busara itumike ya kuwataka wavae nguo ili wasikilizwe kero zao.
mahabusu hao wamedai kuwa hawana nia ya kufanya fujo na kwakuwa serikali sikivu wanaomba kusaidiwa.
Katibu tawala wilaya ya Geita Gasper Kanyaita amechukua majina ya mahabusu hao ili kufatilia mafaili yao na kujua namna ya kuwasaidia.
Baada ya kubembelezwa kwa muda mrefu hatimaye mahabusu wakakubali kurudi gerezani baada ya kuahidiwa kuja kusikilizwa kero zao siku ya leo.
Post a Comment