Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa
China, Mhe. Li Yuanchao (kulia) akiangalia jengo la Makao Makuu ya Ofisi ya
Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) mara baada ya kuwasili Makao
Makuu ya shirika hilo leo jijini Dar es Salaam kwenda kuangalia miundo mbinu
ikiwemo mabehewa na injini za treni za shirika hilo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa
China, Mhe. Li Yuanchao (kushoto) akiangalia ramani ambayo reli ya TAZARA
inapita kuanzia kituo cha Dar es Salaam wakati alipotembelea Makao Makuu ya
Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) leo jijini Dar es Salaam kwa
ajili ya kuangalia miundo mbinu ikiwemo mabehewa na injini za treni za shirika
hilo. Kulia ni Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa
China, Mhe. Li Yuanchao (katikati) akielekea katika moja ya treni ya Shirika la
Reli la TAZARA kwa ajili ya kuelekea katika moja ya kituo cha Mizigo cha treni
ya TAZARA kilichopo Yombo jiji Dar es Salaaam.
Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison
Mwakyembe (katikati) akiwa amekaa ndani ya moja ya treni ya abiria tayari
kuelekea katika kituo cha Mizigo cha treni ya TAZARA kilichopo Yombo jiji Dar
es Salaaam. Kulia ni mgeni wake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China,
Mhe. Li Yuanchao.
Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison
Mwakyembe akishuka toka ndani ya treni ya abiria ya TAZARA kuelekea katika
kituo cha mizigo cha TAZARA kilichopo mtaa wa Yombo jijini Dar es Salaam.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao akishuka toka ndani ya
treni ya abiria ya TAZARA kuelekea katika kituo cha mizigo cha TAZARA kilichopo
mtaa wa Yombo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupatiwa maelezo ya kina
kuhusiana na reli hiyo
Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison
Mwakyembe (kushoto) akimpa maelezo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China,
Mhe. Li Yuanchao (kulia) kuhusiana na shughuli zifanywazo na kituo cha
kuhifadhia mizigo inayobebwa na treni ya Shirika la TAZARA wakati alipotembelea
katika kituo hicho leo jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa
China, Mhe. Li Yuanchao (kushoto) akimshukuru Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison
Mwakyembe (kulia) mara baada ya kupata maelezo mazuri kuhusu kazi zifanywazo na
Makao Makuu ya Shirika la TAZARA.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa
China, Mhe. Li Yuanchao (wa pili toka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na
mwenyeji wake Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe (kulia) mara baada ya
kukamiliha ziara ya kutemebelea Makao Makuu ya Shirika la Reli la Tanzania na
Zambia (TAZARA) leo jijini Dar es Salaam.PICHA ZOTE
NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.
Post a Comment