Akiwa angani: Obama akitazama mechi ya mwisho ya Marekani dhidi ya Ujerumani akiwa kwenye ndege yake.
RAIS
wa Marekani, Barack Obama ameonesha jinsi gani kombe la dunia ni muhimu
kwa taifa lake baada ya kuamua katazama mchezo wa mwisho wa kundi G
dhidi ya Ujerumani akiwa kwenye ndege yake binafsi.
Obama
alikuwa anasafiri kwa ndege kutoka Maryland kwenda Minnesota
wakati Marekani ikicheza mchezo muhimu na alihakikisha hakosi mchezo huo
kupitia matangazo ya moja kwa moja kwenye luninga iliyopo kwenye ndege
yake.
Kitu kwa anga: Obama akitazama mechi ya Marekani na kushuhudia taifa lake likifuzu hatua ya 16.
Mashabiki wa timu ya taifa ya Marekani walishangilia timu yao wakiwa kote Marekani na Brazil.
Kikosi
cha Mjerumani, Jurgen Klinsmann kilipoteza mechi kwa goli la Thomas
Muller, lakini kimefuzu hatua ya mtoano kwa wastani mzuri wa mabao ya
kufunga na kufungwa dhidi ya Ureno.
Klinsmann alichapisha barua ya kuomba sapoti kutoka kwa mashabiki wa Marekani na viongozi kwa ujumla.
Ruksa: Gavana wa New York , Andrew Cuomo alijibu maombi ya Klinsmann kwenye mtandao wa Twita.
Post a Comment