Jeshi
la polisi mkoani Kilimanjaro linawashikilia watu wawili wanaoshukiwa
kuwa majambazi ambao walikutwa wakiwa na bunduki mbili aina ya shortgun
zikiwa zimekamatwa vitako huku moja ikiwa imefungiwa hirizi kama kinga
ya kuzuia wasikamatwe katika matukio ya uhalifu.
Kamanda
wa polisi mkoani Kilimanjaro Bw Robert Boaz amesema, watu hao Ibrahimu
Machaku na Laurenti Massawe wamekamatwa juzi na jana katika oparesheni
maalum ya kupambana na matukio ya uhalifu ambapo pia walifanikiwa
kukamata kilo 4.5 za dawa za kulevya aina ya Cocain kwenye uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro.
Kamanda
Boaz amewaambia waandishi wa habari kuwa Massawe ambaye ni mkazi wa
Arusha pia alikamatwa akiwa na vitu vya dhahabu na simu mbili ambavyo
aliporwa mfanyabiashara mmoja mjini Moshi Bw Mehboob Sadiki baada ya
kuvunjwa nyumba yake Juni 22.
Amesema,
katika oparesheni hiyo polisi walikamata dawa hizo zikiwa zimetelekezwa
na abiria aliyekuwa akisafiri na ndege kutoka Brazil kupitia Ethiopia,
Mombasa hadi kwenye uwanja huo na jeshi la polisi limeanza kumsaka
abiria huyo ambaye alitoweka.
Post a Comment