Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TAARIFA YA KANUSHO KWA UMMA KUTOKA SHIRIKA LA MAENDELEO YA PRTEOLI TANZANIA( TPDC) KUHUSU UTAFITI WA MAFUTA NA GESI ASILIA KATIKA MAENEO YA MOROGORO NA KILIMANJARO

 


 Katika toleo Na. 1734 la gazeti la Jambo Leo la tarehe 10 Juni, 2014 katika  ukurasa wa tatu iliandikwa taarifa iliyokuwa na kichwa cha habari  “Utafiti wa gesi kuinufaisha Morogoro, Kilimanjaro”. Taarifa hiyo ilieleza kuwa  wakaazi wa mikoa tajwa watanufaika na ugunduzi wa mafuta na gesi uliofanywa  na Kampuni ya Swala katika maeneo hayo. 
 
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) linapenda kuwafahamisha  wananchi kuwa taarifa ya kwamba Kampuni ya Swala imegundua gesi na mafuta  katika maeneo ya Morogoro na Kilimanjaro sio sahihi. Ugunduzi wa mafuta  hufanyika tu baada ya kuchimba kisima cha utafiti na hatimaye mafuta au gesi  iweze kutoka yenyewe kutoka ardhini.
 
 Hatua ya kuchimba kisima cha utafutaji  hutokana na tafiti mbali mbali za awali za mitetemo ya ardhi na kubaini kama  maeneo hayo yana uwezekano wa kuwa na mafuta au gesi ama la. Hata kama  eneo linaonesha dalili nzuri za awali ni lazima sehemu hiyo ichimbwe na matokeo 
yake ni kuwa na ugunduzi au la. Vilevile ugunduzi huo lazima uonyeshe kutoa kiasi cha rasilimali ambacho kinaweza kuzalishwa kibiashara (economically  viable). 
 
Kazi zilizofanyika mpaka sasa na Kampuni ya Swala katika maeneo ya Morogoro   – Kilosa na Pangani - Kilimanjaro ni utafiti wa awali wa kukusanya takwimu za  mitetemo na kubaini kama maeneo hayo yana kina (thickness) cha kutosha cha  miamba tabaka ambayo utafiti wa mafuta na gesi unaweza kufanyika. Hivyo  utafiti wa kina unaendelea ili kubaini kama kuna miamba mashapo (prospects) ya  kutosha kwa ajili ya kuchimba kisima cha utafiti. Uchimbaji wa kisima hicho  unaweza kutoa mafuta au/na gesi au maji matupu. Hatua ya uchimbaji visima  bado haijaanza.Hivyo basi si sahihi kwa mtu yeyote kusema kuwa kuna  ugunduzi uliofanyika. 
 
Utaratibu wa kutafuta mafuta nchini ni wa kugawana mapato kati ya Mwekezaji  na Serikali kupitia Mikataba ya Kugawana Mapato (Production Sharing  Agreement-PSA) kama mafuta au gesi ikigundulika. Kampuni isipogundua  rasilimali yeyote, Serikali haimrudishii Mwekezaji fedha zake alizowekeza kwenye  ufafiti huo, hivyo hasara hiyo ni kwa Mwekezaji mwenyewe. 
 
Shirika lina taarifa kuwa Kampuni ya Swala inauza Hisa zake katika soko la Hisa  la Dar es Salaam ili Watanzania washiriki katika shughuli za utafutaji wa mafuta  na gesi. Suala hili ni jema na Kampuni ya Swala inastahili kupongezwa kwa  kuwawezesha Watanzania kushiriki kwenye sekta hii ambayo imeshika kasi katika  miaka mitatu iliyopita. Aidha, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania  linawashauri Wananchi wafanye maamuzi mazuri na kuwatumia washauri wao  kuhusu ununuzi wa hisa hizo kwa kuzingatia mambo yaliyoelezwa hapo juu. 
 
Ikumbukwe kuwa Tanzania tumechimba visima vya utafiti wa mafuta vipatavyo  78 na vyenye gesi ni asilimia 40% tu huko Mkuranga (Pwani), Songosongo  (Lindi), Ntorya na Mnazi Bay (Mtwara) na Bahari ya kina kirefu. 
 
Taarifa kuwa katika mikoa ya Morogoro na Kilimanjaro kumefanyika ugunduzi wa  mafuta na gesi haina ukweli wowote. Kama rasilimali ya mafuta au gesi asilia  ikigundulika mwenye mamlaka ya kutangaza ugunduzi huo ni Mheshimiwa Waziri  wa Nishati na Madini pekee. 
 
Kwa maelezo zaidi wasiliana na: - 
 
Mkurugenzi Mtendaji, 
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania, 
BWM Tower A, 
S.L.P 2774, 
Dar es Salaam. 
Barua pepe: tpdcmd@tpdc-tz.com
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top