RAIS
wa Barcelona imesisitiza kuwa Lionel Messi "hauziki" wakati huu miamba
hiyo ya katalunya ikihangaika kumuongeza katika kikosi chao Luis Suarez
msimu ujao.
Kwa
sasa Messi anaichezea timu ya taifa ya Argentina katika fainali za
kombe la dunia na ameshafunga mabao manne na kuifikisha hatua ya robo
fainali.
Nyota huyo mwenye miaka 27 siku za karibuni alisaini mkataba na Barcelona ambao utamuingizia paundi milioni 16.3 kwa mwaka.
Rais
wa klabu, Josep Maria Bartomeu alisema: "Nikiwa nahusika moja kwa moja,
Messi hataki kuondoka. Tulimpa mkataba mpya siku si nyingi na ana
furaha".
Kiungo wa Barca , Xavi (kulia) bado hajaamua hatima yake
Bartomeu pia alisema Xavi anaweza kuondoka klabuni hapo, lakini hajaamua bado ataelekea wapi.
"Xavi
ana haki ya kuamua anataka kufanya nini na tutaheshimu suala hilo. Siku
moja atarudi klabuni kwasababu ana uwezo wa kuwa kocha mkubwa".
Barcelona
walishafungua ofa ya paundi milioni 72 siku ya jumatano usiku, lakini
Liverpool wanata mkwanja wa paundi milioni 80 ili kumuuza nyota huyo
mwenye miaka 27.
Post a Comment