BEKI
David Luiz amesema atamudu presha ya kuiongoza nchi hiyo yenye watu
Milioni 200, wakati Brazil itakapomenyana na Ujerumani kesho katika Nusu
Fainali ya Kombe la Dunia.
Beki
huyo wa zamani wa Chelsea atakuwa Nahodha wa timu yake kesho, kufuatia
FIFA kuipilia mbali rufaa ya Thiago Silva kuonyeshwa kadi ya pili
ya njano kwenye michuano ya mwaka huu katika mchezo dhidi ya Colombia
ambao timu yake ilishinda 2-1.
Nyota
kinda wa Brazil, Neymar pia ataikosa Nusu Fainali kwa sababu ni
majeruhi, lakini Luiz anaamini watatinga Fainali itakayochezwa Jumappili
Uwanja wa Maracana.
Beki
huyo wa kati wa Paris St Germain amesema: "Niko tayari. Mimi Nahodha
Msaidizi na kundi hili ni rahisi saran kulimudu kwa sababu kila mmoja ni
mtaratibu. Haitakuwa kazi ngumu kabisa,".
Big Phil: Kocha Scolari akitoa maelekezo kwa vijana wake mazoezini mjini Teresopolis
Luiz akimuonyesha kitu Marcelo
Post a Comment