Diamond Platinumz ametangaza kupitia Instagram kuwa ataachia video mbili kwa mpigo ikiwa ni siku chache baada ya kumalizana na BET Awards 2014.
Mashabiki wake wategemee kuona video mbili kwa wakati mmoja ambazo ni
moja ya wimbo aliofanya na mkali wa Kukere, Iyanya wa Nigeria, na
nyingine ya wimbo wenye asili ya ngoma za kitanzania Kitorondo aliyoipa
jina la MdogoMdogo.
Diamond ameendelea kushare picha mbalimbali kutoka kwenye video hizo,
picha zinazoashiria kuwa video hizo zitakuwa tofauti kabisa na video za
awali za Diamond.
Katika moja ya picha alizoshare Instagram akiwa katika eneo lenye
miamba na maporomoko ya maji huku akiwa amevaa kama mtu anaeishi
nyikani, aliwataka mashabiki wataje uhusika wake.
“Nikikupa Nafasi moja tu ya Kunipa Jina katika Caracter hiyo we
ungenipa jina Gani?..... [ If I was to give you a chance to give me a
name from that character what would it be...?]”
Hata hivyo, bado hajatangaza tarehe rasmi atayoziachia video hizo na amewataka mashabiki kupendekeza tarehe.
Hata hivyo, bado hajatangaza tarehe rasmi atayoziachia video hizo na amewataka mashabiki kupendekeza tarehe.
Post a Comment