Ingawa hayupo Tanzania lakini hakungoja mpaka arudi ndipo akabidhi zawadi hii badala yake alichokifanya ni mara baada ya kukamilisha kila kitu kinachoihusu gari hii Diamond Platnumz aliwapatia mameneja wake kwa ajili ya kuiwasilisha kwa mama yake.
Ni Toyota Lexus New Model ambapo Babu Tale amesema imegaharimi
milioni 38.1 ambapo milioni 35 imetumika kulinunulia gari hilo mpaka
kuingia Tanzania na Milion 3.1 imetumika kulipamba na kuweka Music
System pamoja na seat Cover.
Zawadi hii ameitoa Diamond kwa mama yake kama zawadi kwa ajili ya
kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa mama yake ambaye amesema ametimiza
miaka 55, mama yake amesema hakutegemea zawadi hii na anamuombea mwanae
kwa Mungu afanikiwe zaidi.
Baada ya kufuturu Meneja wa Diamond Babu Tale alitangaza utaratibu wa
kuzindua kwanza video mbili za Diamond kwa watu waliokuwepo hapo kisha
utaratibu mwingine ukaendelea ikiwemo kumuimbia mama yake Diamond kisha
kukabidhiwa gari yake.
Hizi ni picha kuanzia wakati wa kufuturu hadi mama yake Diamond
anakabidhiwa gari hiyo mbele ya mastar kadhaa akiwemo Wema
Sepetu,Shettah,Madee,Profesa Jay,Aunt Ezekiel na wengine kibao.
Millard ayo
Post a Comment