Serikali
imetangaza kuwa haitawaruhusu wahitimu wa elimu ya juu wanaodaiwa na
Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kwenda nje ya nchi kwa masomo
zaidi au kufanya kazi mpaka watakapomaliza kulipa madeni yao.
Akizungumza
bungeni hivi karibuni, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Jenista Mhagama alisema hatua hiyo inalenga kuongeza kiwango cha
ukusanyaji wa mikopo ambayo imeshawanufaisha wahitimu wengi ingawa ni
wachache wanaorejesha.
"Tumezungumza
na idara ya uhamiaji ili wale wote wanaotaka kwenda kufanya kazi nje ya
nchi wasiruhusiwe mpaka watakapomaliza kulipa mikopo yao ya elimu ya
juu. Lengo ni kuepuka ukwepaji unaojitokeza baada ya kuajiriwa,"
alisema.
Suala la
wahitimu wa Kitanzania kutafuta kazi nje ya nchi limekuwa likizungumzwa
na wadau wengi kama njia mbadala ya kupata ajira, kutokana na kuwapo kwa
ushindani mkubwa wa soko la ndani la ajira.
Wahitimu
Hata
hivyo, baadhi ya wadau hawaoni manufaa endelevu ya mpango huo, wakisema
chombo kinachohusika na mikopo hakijajipanga vilivyo kukusanya madeni na
ndiyo maana kimeshindwa kuwafikia hata wadaiwa waliomo nchini.
Leonard
Mhongole ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Ardhi mwaka 2010. Anasema mkakati
huo hauwezi kuleta tija kwa kuwa ni watu wachache sana wanaofikiria
kwenda nje ya nchi.
"Mamlaka
husika zinaangalia sana waajiriwa wa serikalini lakini kwa wale
tunaofanya kazi sekta binafsi au waliojiajiri hatufikiwi. Kama watu wote
watabanwa kama inavyotakiwa nadhani fedha za kutosha zitarudi
serikalini," anasema na kuongeza:
"Mimi
binafsi nilitakiwa niwe nimeanza kulipa mkopo wangu lakini kwa kuwa
hakuna anayenitaka kufanya hivyo siwezi kuwatafuta
wahusika...inawezekana wametoa msamaha kwa baadhi ya watu."
Kwa upande wake, mwanafunzi wa shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Joseph Isindikiro, anas
Post a Comment