Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NUSU FAINALI BRAZUCA, VITA YA WAAMERIKA NA WADACH

      


Brazil-vs-Germany-2014-World-Cup-Semi-finals-Football-Wallpaper-1024x576
Na Baraka Mbolembole

Uholanzi ilifuzu kwa mara ya pili mfululizo nusu fainali ya kombe la dunia baada ya kuwashinda timu ya Costa Rica kwa changamoto ya mikwaju ya penalti dhidi ya Costa Rica katika mchezo pekee wa robo fainali ambao ulichezwa kwa dakika 120 na matokeo kuwa suluhu-tasa.

Sasa ‘ wataalamu wa soka la mbinu’ Ujerumani na Uholanzi watakutana na timu zenye vipaji kutoka ‘ bara la soka’. Kwa mara ya kwanza timu za Brazil na Argentina zimefuzu kwa wakati mmoja hatua ya nusu fainali na mafanikio yametokana na timu hizo kucheza kwa ushirikiano na umakini mkubwa katika michezo mitano iliyopita.

UJERUMANI vs BRAZIL



 Ujerumani waliichapa Ureno kwa mabao 4-0 katika mchezo wa kwanza, baada ya hapo kikosi cha Joachim Loew kimemuda kufunga mabao sita katika michezo minne iliyopita, watacheza na wenyeji, Brazil katika mchezo wa nusu fainali , jumanne hii. Mchezo huo unataraji kuwa mgumu lakini bado safu ya ulinzi ya kikosi cha Ujerumani kinatakiwa kupunguza utegemezi kutoka kwa golikipa, Manuel Neur ambaye alifanya kazi kubwa katika mchezo wa robo fainali dhidi Ufaransa pale alipookoa nafasi za wazi.

Neur anafanya vizuri kazi yake hadi sasa kama golikipa ni lazima afanye vyovyote vile kuhakikisha mpira hauingii golini. Ila, kitendo chake cha kuingia katika majukumu ya ulinzi wa kati katika mchezo dhidi ya Algeria wa hatua ya 16 bora ni kielelezo tosha kuwa safu hiyo ya ulinzi ya ‘ National Eleven’ inapitika kiurahisi pale wanaposhambulia. Low alimuondoa mlinzi, Per Mertesacker na kuwapanga, Mat Hummels na Benedkt Howes katika mchezo wa robo fainali. Hummels alifunga bao pekee katika mchezo huo akiunganisha kwa kichwa mpira wa faulo uliopigwa na Ton Kros, alitajwa kama mchezaji bora wa mechi kutokana na kucheza kama kiongozi wa idara ya ulinzi na kulinda bao hilo kwa dakika 81.. Pamoja na tuzo hiyo kupewa Hummels, golipika, Neur alifanya kazi kubwa kuokoa michomo ya Karim Benzema

article-2681224-1F66B2F100000578-76_634x756

Rafu mbaya iliyochezwa na mlinzi wa Colombia, Juan Zuniga dakika ya 88 imemuondoa Neymar katika michuano japo timnu yake ilifanikiwa kjufuzu kwa mchezo wa nusu fainali. Neymar hatukuwepo katika mchezo dhidi ya Ujerumani siku ya jumanne ijayo, na hatoweza kushiriki katika mchezo wa fainali, julai 13 endapo Brazil itafanikiwa itafanikiwa kufika fainali ya michuano hiyo ya 20. Staa huyo wa Brazil alikuwa kila kitu kwa timu yake katika michezo mitano iliyopita , na alicheza huku akizunguka eneo lote la mashambulizi la Colombia, hakika Brazil itamkosa mchezaji muhimu sana lakini bado mhistoria inawabeba mbele ya Ujerumani, mabingwa mara tatu wa michuano hiyo.

Nahodha na mfungaji wa bao la kwanza la Brazil dhidi ya Brazil, Thiago Silva hatokuwepo katika mchezo ujao kutokana na kupata kadi ya pili ya njano katika mchezo huo walioibuka na ushindi wa mabao 2-1. Kocha wa Selecao atakuwa katika mtihani wake mkubwa zaidi kabla ya kushinda taji lake la pili wakati Brazil itakapokuna na timu iliyocheza mchezo wa nidhamu kubwa na kujilinda katika muda mwingi wa mchezo wa robo fainali dhidi ya Ufaransa.

Ujerumani imefuzu nusu fainali yake ya nne mfululizo na kuwa timu ya kwanza kufanya hivyo, itakuwa ikiweka rekodi nyingine ya michuano ya timu iliyocheza michezo mingi zaidi mfululizo ya michuano hiyo. Mchezo dhidi ya Brazil utakuwa ni wa 27 hivyo watakuwa wakivunja rekodi ya Brazil ambao walicheza michezo 26 mfululizo ya michuano hiyo. Selecao ilicheza michezo yote saba ya michuano kuanzia fainali za mwaka 1994, 1998, 2002 na waliishia robo fainali mwaka 2006 walipofungwa na Ufaransa, timu ambayo safari hii imeshindwa kuwazuia Ujerumani baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0. Scorali atakuwa katika mtihani mkubwa katika kufanya machaguo ya wachezaji wa kuanza katika mchezo dhidi ya ‘ National Eleven’. 

hi-res-c86a6fd93e932abdf89d9d6335bbd6cf_crop_northMIPAMBANO YA NYUMA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 10 ILIYOPITA

Adriano Leite alifunga bao la kuongoza kwa Brazil katika dakika ya 21, Lukas Podolski akasawzisha dakika mbili baadae na kufanya matokeo kuwa bao 1-1. Dakika ya 43, Ronaldinho Gaucho akafunga bao la pili kwa mkwaju wa panalti, dakika mbili baadae nahodha wa zamani wa Ujerumani, Michael Ballack akasawazisha kwa njia ya penalti na kufanya timu hizo kuwa sare ya mabao 2-2 katika nusu ya kwanza ya mchezo wa nusu fainali wa kombe la Mabingwa wa Mabara, juni, 25, 2005,jijini Berlin. Ushindi huo ni wa mwisho kwa Brazil dhidi ya Ujerumani katika kipindi cha muongo mmoja sasa.

Ushindi wa mabao 3-2 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki ambao Ujerumani iliupata, agosti, 2011 ndiyo pekee ambao wamewahi kuupata katika kipindi cha miaka 14 iliyopita. Wakati mchezo wa mabingwa wa mabara ulitoa mabao manne katika kipindi cha kwanza tu huku mikwaju miwili ya penalti ikitumika, katika mchezo mabao yote matano yalifungwa katika muda wa dakika 30 za mwisho. Kiungo Bastian Schweinsteiger alifunga bao la kuongoza kwa njia ya mkwaju wa penalti, Mario Gotze akaoneza bao lingine dakika sita baadae.

Robinho alifunga bao la kwanza la Brazil kwa njia ya penalti katika dakika 71, kabla ya Andre Schurrle kufunga bao la tatu dakika ya 80 na kufanya Ujerumani kuongoza kwa mabao 3-1. Neymar alifunga bao la pili la Selecao katika dakika ya mwisho ya mchezo huo uliomalizika kwa Brazil kulazwa mabao 3-2. Mchezo pekee ambao ulimalizika kwa sare baina ya timu hizo ni ule wa , septemba, 2004 wakati, mshambulizi, Kelvin Kuranyi aliposawazisha katika dakika ya 17 akifuta bao la mepema dakika ya tisa lililofungwa na Gaucho. Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya kufunga bao 1-1.

article-0-1E861D8000000578-483_306x423

BRAZIL INAITESA UJERUMANI KATIKA KOMBE LA DUNIA

Ujerumani walicheza kwa kujiamini dhidi ya Ufaransa hata pale walipokuwa katika wakati mgumu hiyo ndiyo tabia alisi ya wachezaji wa Ujerumani kizazi hadi kizazi . Wachezaji wan chi hiyo wamekuwa wakiongozwa na historia nzuri ya vikosi vilivyopita na wameendeleza hilo katika fainali zinazoendelea nchini Brazil.. Kocha Loew aliamua kumuacha nje mlinzi wa Arsenal, Per Mertesacker na kumpanga Benedikt Howes kutoka na Per kutokuwa na kasai na udhaifu huo uliwafanya kupata shida katika mchezo wa hatua ya 16 bora dhidi ya Algeria.

David Luiz alifunga ‘ bao la nguvu na la aina yake’  atamkosa patna wake Silva lakini nafasi hiyo inataraji kuzibwa na mlinzi wa Bayern Munich, Dante ambaye hajacheza mchezo wowote katika michuano. Nafasi hiyo inaweza kuzibwa lakini ‘ Big Phill’ atalazimika kufanya mabadiliko katika safu ya mashambulizi kwa kuwas amempoteza mchezaji wake bora zaidi kikosini, Neymar. Brazil inaweza kubebwa na mshambulizi, Hulk ambaye amekuwa akitumika zaidi kama kiungo wa mashambulizi akitokea pembeni. Hulk ni mshambulizi na mfungaji mahiri wa kati, ila kiwango cha chini ambacho kimeendelea kuoneshwa na Fred ni tatizi kubwa kwa Brazil kwa kuwa JO, mshambulizi mwingine wa nyongeza katika kikosi hana kasi na ‘ mlaini’ sana.

Timu hizo zimewahi kukutana mara moja katika michezo ya kombe la dunia. Brazil ilitwaa ubingwa wake wa mwisho wa dunia mwaka 2002 baada ya kuichapa Ujerumani kwa mabao 2-0 yaliyofungwa na Ronaldo De Lima katika uwanja wa Yokohama, Japan. Baada ya hapo kikosi hicho kimefundishwa na makocha wqatatu tofauti, Carlos Alberto Perreira ambaye aliipeleka timu hiyo hadi katika robo fainali katika fainali za mwaka 2006, na chini ya Carlos Dunga timu hiyo iliishia tena robo fainali katika fainali za mwaka 2010. Baada ya kuondoka, Dunga, Selecao ilimpata mwalimu, Mano Menezes ambaye aliingoza timu hiyo kwa miaka mitatu kabla ya kumuachia, Scorali mapema mwaka jana.

ac9ef595-63ae-40c9-9ee0-95ac232b3ea4-620x372

Ujerumani imekuwa chini ya Joachim Loew tangu mwaka 2006, lakini mwalimu huyo alikuwa msaidizi wa Jurgen Klinsmann kwa miaka miwili kabla ya kupewas mikoba rasmi ya kuinoa timu hiyo. Loew amekuwa sehemu ya kombe la dunia katika michuano miwili iliyopita na mara zote alishuhudia kikosi cha kikiondoshwa katika nusu fainali. Mwaka 2006 walipokuwa wenyeji walifungwa pasipo kutarajiwa na Italia, na mwaka 2010 walifungwa na Hispania na timu zote hizo zilifanikiwa kutwaa taji katika michezo ya fainali.

Brazil haijawahi kupoteza mchezo wa nusu fainali wa kombe la dunia, wakati Ujerumani imepoteza mara nne.  Kipa wa Ujerumani, Manuel Neur aliokoa nafasi tano za wazi katika mchezo war obo fainali dhidi ya Ufaransa katika mchezo ambao safu yake ya ulinzi ilipokea mashambulizi 13 huku mipira tisa ya hatari ikifika langoni. Timu ambayo ilianza michuano kwa kuitandika Ureno mabao 4-0 ilishambulia mara nane tu huku mashambulizi sita yakiwa ya uhakika. Ujerumani imeendelea kuwa timu ya michuano na itawabidi kugangamara hasa ili kuvuka hatua ya nusu fainali mbele ya Brazil ambao wamefunga mabao kumi katika michezo mitano iliyopita.

Wakati kikosi cha Loew kilicheza faulo 18 na wachezaji wake wawili kuonyeshwa kadi za njano, Selecao ilikuwa na siku nzuri japo ilishuhudia mshambulizi wake namba moja akiumia dakika mbili kabla ya kumalizika kwa mchezo war obo fainali. Brazil imekuwa timu yenye nguvu katikati ya uwanja na katika safu ya nyuma. Ikiwa imeruhusu mabao matatu hadi sasa, timu hiyo ilicheza faulo mara 31 huku wakipokea mashambulizi mara 11. Itampokea tena kiungo wake wa ulinzi, Luis Gustavo ambaye alikuwa akitumikia kadi katika mchezo war obo fainali. Tofauti na Ujerumani ambao walimiki mpira kwa asilimia sawa na Ufaransa-50+50, vijana wa Big Phill walimiki mpira kwa asilimia moja zaidi ya timu ambayo ilikuwa ikiogopewa sana katika michuano ya mwaka huu.

0714 08 43 08
 
Imechotwa: shaffihdauda.com
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top