Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Ombi kwa facebook dhidi ya binti mdogo aliyeua chui na wanyama wengine wakali.

bintichui
Baadhi ya watumiaji wa mtandao wa Facebook wameanzisha kampeni kubwa kuitaka kampuni hiyo kuondoa picha za binti mdogo mwindaji anayeonekana amepiga picha na wanyama wakali anaodai kuwaua katika nchi za kiafrika ikiwemo Zimbabwe.
Binti huyo Kendall Jones kutoka Cleburne, Texas, anadaiwa kuwa ni mwindaji mdogo zaidi kuwapiga risasi wanyama hao wakali wa mwituni akiwemo Chui na kuthibitisha hilo amekuwa akipozi nao kwa picha baada ya kufanya kitendo hicho.
bintichui2
 
Maelfu ya watu wanaitaka Facebook kuondoa picha hizo ambapo binti huyo amejitetea kuwa anafurahi kuendeleza ndoto zake.
bintichui3
Lakini pia binti huyo ameandika kupitia akaunti yake ya Facebook kuwa anatarajia kuanzisha kipindi chake cha Televisheni ifikapo mwaka 2015.
Binti huyo amekuwa akitabasamu na kuweka pozi pembeni ya wanyama wa aina mbalimbali anaodai kuwaua ambapo picha hizo zimeamsha hisia kali katika mitandao ya kijamii watu wakidai ziondolewa.
Mmoja wa mashabiki amenukuliwa akisema kuwa”Kwa vyovyote vile utakavyoangalia, kuona mtu anatabasamu pembeni ya mwili uliokufa ni kitendo cha kuhuzunisha sana.”
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top