Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Palestina ipo tayari kusitisha mapigano


Uharibifu uliofanywa Gaza kutokana na vita
Uongozi wa Palestina umependekeza makubaliano ya saa ishirini na nne ya kusitisha mapigano dhidi yake na Israel.
Yasser Abed Rabbo wa chama cha PLO, Palestine Liberation Organisation amesema mpango huo umeungwa mkono na makundi muhimu likiwemo kundi la Hamas na la Islamic Jihad.
Hata hivyo mmoja wa maafisa wa Hamas Abu Zuhri amesema taarifa hiyo ya PLO haiwakilishi upande wa Hamas.
Mapema pendekezo la makubaliano ya kusitisha mapigano lililotangazwa, halikuweza kutekelezwa kwa kuwa hakuna upande wowote ulioweza kulitekeleza kwa kusitisha mapigano katika eneo la Gaza.

Bwana Rabbo amesema ujumbe wa pamoja unaoongozwa na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas utakwenda Cairo kuweka masharti ya kusitisha mapigano.CHANZO BBC SWAHILI
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top