Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI YATOA FURSA YA MIKOPO KWA WANAFUNZI WATAKAOJIUNGA NA MASOMO YA STASHAHADA YA UALIMU




Frank Mvungi_ Maelezo.



Serikali  imetoa fursa ya mikopo kwa wanafunzi watakaojiunga na masomo ya stashahada maalum ya ualimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati.


Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Habari Elimu na Mawasiliano toka Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya Juu Bw. Cosmas Mwaisobwa wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari Leo Jijini Dar es salaam.



“ Wanafunzi wapatao 5,000 wanatarajiwa kujiunga na stashahada maalum katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambapo wote watanufaika na mikopo ya elimu ya Juu.”Alisema Mwaisobwa.




Akifafanunua, mwaisobwa alisema kuwa lengo la mpango huo ni kusaidia kuondoa tatizo la walimu wa masomo ya sayansi hapa nchini . Aidha Mwaisobwa alibainisha kuwa jumla ya maombi 58,037 ya mikopo  yalikuwa yamepokelewa hadi kufikia Julai 2014 ambapo maombi 37,689 ni waombaji wa kiume na 19,592 ni waombaji wa kike.



Pia Mwaisobwa alibainisha kuwa majina ya wanafunzi watakaopata mikopo kulingana na udahili yatatangazwa kwenye tovuti ya Bodi  ambayo ni www.heslb.go.tz.na taarifa hiyo itatangazwa katika vyombo vya habari.



Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu (HESLB) inakusanya wastani wa shilingi bilioni 3 kwa mwezi ikiwa ni marejesho ya mikopo iliyokwisha tolewa.

WAKATI HUO HUO  

 



Serikali imesema ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya fedha za malipo ya mafunzo kwa vitendo kwa mwaka wa masomo 2013 2014.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi Habari, Elimu na Mawasiliano Cosmas Mwaisobwa wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.

Mwaisobwa alisema kuwa jumla ya wanafunzi  9946 kutoka vyuo vikuu vitano hawajapatiwa fedha kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo ambao wengi wao tayari wako katika maeneo waliyopangiwa.

“Bodi tayari imeandaa malipo yao na yanatarajiwa kutumwa mwishoni mwa juma hili, ambapo vyuo vikuu vitano  ikiwemo Tumaini Makumira (TUMA) wanafunzi 1 715, Stefano Moshi (SMMUCO) wanafunzi 1 191, Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM)wanafunzi 2 578,  Mt. Augustino (SAUT) wanafunzi 2639 na Teofilo Kisanji (TEKU) wanafunzi 1823.

Akijibu swali la waandishi wa Habari Mwaisobwa alisema kuwa sababu zilizopelekea kuchelewa kwa fedha hizo ni mchakato wa upatikanaji wa fedha  zilitarajiwa kupatikana mapema zaidi.

Aidha, Mwaisobwa alitoa rai kwa wazazi na walezi wenye uwezo wa kuwalipia watoto wao wafanye hivyo ili kuwapa nafasi wale wasio na uwezo wa kunufaika na mkopo mkopo wa Bodi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top