Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

JUMUIYA YA WAZAZI CCM MKOA WA DAR ES SALAAM, YAZINDUA DAFTARI LA WANACHAMA.

 

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Seif Shaban Mohamed (kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Daftari la wanachama wa Jumuia hiyo mkoa wa Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Seif Shaban Mohamed (kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Daftari la wanachama wa Jumuia hiyo mkoa wa Dar es Salaam

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Seif Shaban Mohamed (kushoto) na Katibu wa Jumuia hiyo mkoa wa Dar es Salaam, Cholaje wakionyesha daftari hilo baada ya kuzinduliwa.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Seif Shaban Mohamed (kushoto) na Katibu wa Jumuia hiyo mkoa wa Dar es Salaam, Cholaje wakionyesha daftari hilo baada ya kuzinduliwa.
Wajumbe wa Kamati ya Afya, Maafa na Mangira wakijadiliana jambo, Kutoka kushoto ni Ali Said, Josephat Kadiya na Dk. Meshack Sabaya.
Wajumbe wa Kamati ya Afya, Maafa na Mangira wakijadiliana jambo, Kutoka kushoto ni Ali Said, Josephat Kadiya na Dk. Meshack Sabaya.
Wajumbe wa Kamati ya Uchumi, Fedha na Mipango, wakifuatilia uzinduzi huo.
Wajumbe wa Kamati ya Uchumi, Fedha na Mipango, wakifuatilia uzinduzi huo.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Seif Shaban Mohamed, amewataka viongozi wa jumuia hiyo kuwa wabunifu wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuifanya jumuia hiyo kukua kiuchumi.
Mohammed ametoa agizo hilo leo, wakati akizindua Daftari la Wanachama wa Jumuia hiyo Mkoa wa Dar es Salaam, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Arnatouglou, mkoani humo.
“Nawapongezeni kwa kuunda kamati ndogondogo ndani ya jumuia, kufanya hivi kuutasaidia kusogeza huduma kwa wanachama wetu na wananchi kwa ujumla hivyo kukifanya chama chetu kiendelee kuaminiwa” alisema Mohamed.
Alisema Jumuia inazo rasimali nyingi hivyo ni vizuri sasa zikatumika ipasavyo kukuza uchumi wa jumuia ya Wazazi na viongozi wa jumuia wasipende kusubiri kila kitu muelekezwe na viiongozi wa juu.
Alitoa mfano wa kitegauchumi cha Jumuia hiyo kilichotelekezwa bila kuendelezwa kuwa nieneo la shule ya jumuia hiyo ya Boza iliyopo mkoani Tanga, ambapo alisema  kuwa ina ardhi ya kutosha lakini haifanyiwi uzalishaji mali wowote.
Mohamed alipongeza Jumuia hiyo Mkoa wa Dar es Salaam kwa kuanzisha daftari hilo la wanachama akisema litasaidia kuwatambua wanachama wao kuanzia ngazi ya shina hadi mkoa hivyo kurahisisha shughuli za kisiasa kwa kutambuana katika chaguzi mbalimbali na shughuli nyingine kama za maendeleo.
Katika hatua nyingine Mohamed alisema wanajumuia wote ya wazazi wanaiunga mkono Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalumu la Katiba na kuwa wao wanautaka muundo wa serikali mbili kwani ndio utalipeleka mbele Taifa la Tanzania.
Alitoa mwito kwa wanachama wote wa CCM kujitokeza kwa wingi kupiga kura ya kuwachagua viongozi wao kuanzia ngazi za mashina wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika hivi karibuni.
Katibu wa Jumuia hiyo mkoa wa Dar es Salaam, Cholaje Ali, alisema mpango wa kuanzisha daftari hilo ni moja ya mikakati yao ya kuibadilisha jumuia kiutendaji.
“Hii jumuia yetu kwa muda mrefu ilikuwa nyuma kimaendeleo lakini tumedhamiria kuibadilisha na kuwa ya kiutendaji zaidi na ndio maanna tumeanzisha kamati ndogo ndogo za maendeleo na kuwateua watu wenye sifa za kuziongoza yaani wenye taaluma” alisema Cholaje
Aliwataka viongozi wote waliochaguliwa kujitambua kuwa wamechaguliwa si kwa bahati mbaya bali ni kwa ajili ya kuonekana kuwa wana uwezo wa kuleta maendeleo ndani ya jumuia hiyo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright 2025 EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG | Designed By Code Nirvana