JESHI la
Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatarajia kuzindua mashindano
ya michezo mbalimbali kwa lengo la kuwashirikisha wananchi wa rika
zote na itikadi mbalimbali
yatakayojulikana“KAMISHNA KOVA CUP”.
Madhumini
ya mashindano haya ni ni Kuwaunganisha wananchi wenye itikadi
mbalimbali ili kupitia
mashindano haya watakaoshiriki watajifunza masuala ya usalama,
uzalendo na kuzingatia utaifa kwa madhumuni ya kuwashirikisha
kikamilifu katika ulinzi wa nchi na kudumisha
amani na utulivu katika jiji la Dar es Salaam na mikoa
mingine.
Lengo
lingine ni Kuishirikisha jamii kuondokana na dhana ya kutenda uhalifu
wa aina mbalimbali kama vile ujambazi, matumizi ya aina mbalimbali
ya madawa ya kulevya, wizi katika mitandao,uzururaji, na kukaa katika
vijiwe bila kazi.
Pia Kupitia
michezo mbalimbali, jamii itafaidika kupata elimu juu ya umuhimu wa
jukumu la msingi la kushiriki katika ulinzi na
usalama wa nchi hii, itakuwa ni fursa nzuri kujua madhara ya
kujihusisha na vitendo vya uhalifu.
Katika
michezo watajifunza kujenga au kuimarisha mahusiano mema baina ya Jeshi
la Polisi na jamii kwa ujumla kupitia dhana ya Polisi Jamii
itatekelezwa kwa vitendo.
Post a Comment