Aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha CUF taifa, Profesa Ibrahimu Lipumba akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kung'atua rasmi umwenyekiti wa chama hicho na kuendelea kuwa mwanachama wa kawaida wa chama hicho.
Lipumba amesema ataendelea kuwa mwanachama halali kwani kadi yake ya uanachama ameshailipia mpaka mwaka 2020.Ameyasema hayo katika ukumbi wa mikutano wa Peacock hoteli jijini Dar es Salaam leo.
Aliyekuwa Mwenyekiti
wa chama cha CUF taifa, Profesa Ibrahimu Lipumba akiwa na wananchi wa
kawaida kulia, Abdala Shabani pamoja na mdogo wake,Shabaani Miraji
wakiwa wamemsindikiza aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF taifa ili kuzungumza
na waandishi wa habari kwa niaba ya wananchi katika mkutano uliofanyika
katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam leo.
Waandishi
wa habari wakimsikiliza Aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha
CUFtaifa, Profesa Iblahimu Lipumba akitangaza kujiuzulu wadhifa
wake katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya
Peacock jijini Dar es Salaam leo.
Aliyekuwa Mwenyekiti
wa chama cha CUF taifa, Profesa Ibrahimu Lipumba akionyesha Rasimu ya
Katiba pendekezwa ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kuwa ndio
iliyosababisha kuungana na kuunda umoja wa katiba ya wananchi
(UKAWA) katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli
ya Peacock jijini Dar es Salaam leo.
Aliyekuwa Mwenyekiti
wa chama cha CUF taifa, Profesa Ibrahimu Lipumba akionyesha Katiba ya
Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo katika mkutano wa kujivua
uenyekiti wa chama cha CUF leo jijini Dar es Salaam.
MWENYEKITI wa Taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF),Profesa Ibrahim Lipumba amejiuzulu nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho leo majira ya saa 5 asubuhi katika Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam.
Akizungumza mbele ya waandishi habari,Pro.Lipumba amesema ametafakari sana katika kuendelea kuwa Mwenyekiti wa chama hicho lakini dhamira yake inamsuta.
Amesema kuwa mwaka 2014 hakutaka kugombea nafasi hiyo kutokana na mchakato wa katiba mpya akaamua kugombea kwa lengo ya kuwapa watanzania katiba itakayoindoa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Lipumba amesema katika mchakato wa bunge maalumu wakaunda umoja wa katiba (UKAWA) wenye lengo wa kusimamia katiba iliyopendekezwa lakini sasa waliopitisha ndio wanataka kuisimamia katiba hiyo ambayo haingii akilini.
Amesema alikuwa akishiriki vikao vya UKAWA lakini Aprili 1 mwaka huu alisema atang'atuka katika nafasi ya uenyekiti wa Chama cha Wanannchi (CUF).
Amesema amepita katika misukosuko mingi katika kukijenga chama hadi kufikia kiasi hata kabambikiziwa kesi ya kufanya maandamano bila kibali.
Lipumba amesema kazi yake atakuwa mwanachama wa kawaida, kufanya utafiti wa maendeleo endelevu pamoja na kufanya ushauri wa masuala mbalimbali katika chama hicho.




Post a Comment